AFARIKI NDANI YA INTERNET CAFE AKICHEZA GAME SIKU TATU MFULULIZO

PANews BT_P-421b8edd-d3a1-4e58-b77a-e18bdc44a141_I1 (1)Vyombo vya habari kutoka Taiwan vimeandika story hii ambayo ni majonzi makubwa, mtu mmoja amefariki katika mazingira ambayo sio rahisi kutegemewa kutokea.


Michezo ya kwenye computer ambayo humpa nafasi mchezaji kucheza online ni maarufu sana Taiwan, watu wengi huipendelea kwa sababu ya unafuu wa gharama pia za mchezo huo.

Hsieh amefariki ndani ya internet cafe baada ya kupata ghafla tatizo la moyo, hiyo ni kutokana na ripoti ya Hospitali, camera za CCTV zinamuonyesha kuwa alikaa kucheza game hiyo kwa saa 72, sawa na siku tatu mfululizo.

Wahudumu wa cafe hiyo wamesema ilikuwa kawaida ya Hsieh kucheza game kwa muda mrefu, akichoka huwa analaza kichwa kwenye meza hivyo hata wakati amefariki walihisi kwamba amelala kama kawaida yake.
Taiwan
Huyu anakuwa mtu wa pili kufariki kwenye internet cafe, wa kwanza alifariki New Taipei baada ya kucheza game kwa siku tano mfululizo.


Bonyeza hapa Tukupe habari zote mara tu Tunapozitoa "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post