Hali hiyo imemkuta Mwanamme Masanja Jilala(38) mkazi wa Maganzo wilayani Kishapu mkoani Shinyanga ambaye amefariki dunia baada ya kunaswa na nyaya za umeme wakati akijaribu kuiba nyaya hizo.
Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga Longinus
Tibishubwamu amesema tukio hilo limetokea jana saa moja na dakika 15 asubuhi katika kijiji na kata
ya Mwadui –Luhumbo wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga.
Anasema mwanamme huyo alifariki dunia baada ya kunaswa na nyaya za umeme
wakati akijaribu kuiba nyaya hizo aina ya Copper zilizokuwa zimechimbiwa
ardhini.
Na Kadama Malunde-Shinyanga
Social Plugin