Hatariii!! MAMA MJAMZITO AJIFUNGULIA KWENYE PARKING YA MAGARI

Parking Lot Sign-313x235
Mwanamke anapokuwa mjamzito hasa unapofika wakati wa kukaribia kujifungua huwa makini sana ili aweze kujifungua salama, lakini kuna wakati ambao hujikuta ana changamoto kutokana na mazingira ambayo uchungu wa kujifungua unampata.
Hii inasikitisha kutokana na kitendo cha mama mmoja kujikuta akilazimika kujifungua katika eneo la parking ya magari nje ya Club kutokana na kupata uchungu akiwa kwenye taxi iliyokuwa ikimpeleka hospitali Tennessee, Marekani.
Maafisa wa zimamoto walipofika eneo la tukio walimkuta mwanamke huyo mwenye umri wa miaka 31 akiwa tayari amejifungua na amempakata mtoto wake ndani ya taxi hiyo.
Baadaye mama na mtoto wake walipelekwa Hospitali ya St. Thomas Midtown.
Meneja wa Club ambayo mtoto huyo alizaliwa kwenye eneo la parking amesema wana mpango wa kumpa zawadi mwanamke huyo pamoja na mtoto wake kiasi cha dola 500 pamoja na zawadi nyingine mbalimbali pamoja na toy za kuchezea.


Mpenzi Msomaji,Tunapenda kukutumia Habari zetu zote mara tu Tunapoziweka Mtandaoni.Kujiunga nasi Bonyeza Hapa "HABARI" VITUKO "MAPENZI"MAGAZETI,UDAKU>
Endapo una Habari,Picha,Video,Tangazo au Tatizo Lolote wasiliana nasi kwa namba  +255 688 405 951

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post