REPOTI YA PAC KUHUSU AKAUNTI YA TEGETA ESCROW YAWASILISHWA BUNGENI DODOMA JIONI HII ,IKO HAPA

Mwenyekiti wa kamati ya hesabu za serikali(PAC) amewasilisha ripoti ya sakata ya Escrow katika mkutano wa 16/17,kikao cha 17 bungeni Dodoma.


ZITTO: Kamati imebaini kuwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwa barua yenye Kumb Na. AGCC/E.080/6/70 ya tarehe 18 Novemba, 2013 alimthibitishia Gavana kuwa hakukuwa na kodi ya Serikali katika fedha zilizokuwa kwenye Akaunti ya Tegeta ESCROW na kwamba fedha hizo zihamishiwe IPTL ili Serikali ijinasue na mashauri yasiyo na tija kwake.


Kutokana na mahojiano kati ya Kamati na Kamishina Mkuu wa TRA ilibainika kwamba Kampuni ya Piper Links haijulikani sio tu British Virgin Islands bali hata nchi nyingine. 


Kamati haielewi ni jinsi gani taasisi kubwa kama Benki Kuu ya Tanzania, Wizara ya Nishati na Madini, Wizara ya Fedha, Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali na nyingine zilizohusika katika suala hili, na ambazo tunaamini zimesheheni Watendaji wenye weledi, zimewezaje.


Wakati mahojiano ya Kamati na Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali, Kamishna Mkuu wa TRA pamoja na Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU tarehe 19 Novemba, 2014 waliithibitishia Kamati kuwa kutokana na makubaliano wa Akaunti ya Tegeta ESCROW, sehemu ya fedha au fedha yote katika Akaunti hiyo ilikuwa ni fedha ya umma.


FILIKUNJOMBE: Kamati imethibitisha bila chembe ya mashaka kwamba mchakato mzima wa kutoa fedha katika akaunti ya Tegeta ESCROW uligubikwa na mchezo mchafu na haramu wenye harufu ya kifisadi ulioambatana na udanganyifu wa hali ya juu ambao kwa kufuata sheria tu ungeweza kugundulika na kuzuiwa.


BONYEZA MANENO HAYA KUSOMA RIPOTI YA ESCROW ILIYOWASILISHWA NA ZITTO KABWE BUNGENI

Kama unaona usumbufu kufungua hiyo Link basi Haya hapa ndiyo Mapendekezo ya KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC) yaliyotolewa jioni hii Bungeni

3.2 Kamati inapendekeza kama ifuatavyo: -
3.2.1 Mheshimiwa Spika, Taasisi ya Kuzuia na kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) na Mkurugenzi wa Makosa ya Jinai (DCI) mara moja
wachukue hatua ya kumkamata Bwana Harbinder Singh Sethi na
kumfikisha mahakamani kwa makosa ya Anti money laundering,
ukwepaji kodi na wizi. Kamati pia inaelekeza Serikali kutumia
sheria za Nchi, ikiwemo sheria ya ‘Proceeds of Crime Act’
kuhakikisha kuwa Bwana Harbinder Singh Sethi anarejesha fedha
zote alizochota kutoka Benki Kuu ya Tanzania. Kwa kuwa suala hili
ni suala la utakatishaji wa fedha haramu, Mamlaka ziwasiliane na
mamlaka za Nchi nyingine kuhakikisha mali za Bwana huyu
zinakamatwa na kufidia fedha hizo.97
3.2.2 Mheshimiwa Spika, Kamati imethibitsha kuwa Bwana James
Rugemalira aliuza hisa ambazo Kampuni yake ya VIP inamiliki
katika IPTL na kulipwa na Bwana Sethi kutoka katika Fedha za
Akaunti ya Tegeta ESCROW. Kamati imethibitisha kuwa fedha
kutoka akaunti za Kampuni ya PAP katika Benki ya Stanbic
zilizofunguliwa maalumu kwa ajili ya kupokea fedha kutoka
Akaunti ya Tegeta ESCROW iliyokuwa Benki Kuu zilipelekwa katika
Akaunti nambari 00151002368801 na Akaunti nambari
00151002368802 za Kampuni ya VIP ziliyopo Mkombozi
Commercial Bank.
Kwa mujibu wa Taarifa ya CAG na kuthibitishwa na Mkurugenzi
Mkuu wa TAKUKURU fedha hizo pia ziligawiwa kwa watu
mbalimbali binafsi. Kamati haina tatizo na watu wawili kuuziana
makampuni yao kwa thamani wajuazo wenyewe, au jinsi ya
kuzitumia fedha zao, ama kuwachagulia watu wa kuwagawia,
lakini Kamati imejidhihirishia kuwa fedha iliyotumika kulipia
manunuzi hayo ni fedha ambayo sehemu yake ni ya umma
iliyochotwa bila huruma wala aibu, kutoka Benki Kuu. Hivyo,
Kamati inazitaka mamlaka za uchunguzi kuhakikisha kuwa fedha
hizo zinarudi Benki Kuu hata ikibidi kwa kufilisi mali za watu wote 98
waliofaidika na fedha hizo kwa thamani ya fedha walizopewa na
Bwana Rugemalira.
Mheshimiwa Spika, baadhi ya waliofaidika na fedha hizo ni
Viongozi wa Umma ambao wanapaswa kuzingatia Sheria ya
Maadili ya Viongozi wa Umma (Sheria namba 13 ya Mwaka 1995)
ambayo inawataka kutoa taarifa ya zawadi wanazopokea au
malipo wanayolipwa. Vyombo vya uchunguzi vifanye uchunguzi
kutambua kama walifuata matakwa ya sheria na hatua mahsusi
zichukuliwe, ikiwemo kuvuliwa nyadhifa zao zote za kuchaguliwa
na/au kuteuliwa, kufilisiwa mali zao na kushtakiwa mahakamani
kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,
ibara ya 132 (1) – (6).
3.2.3 Mheshimiwa Spika, Kamati pia imethibitisha kwamba fedha
zilizolipwa kwa Watu binafsi zilitokana na Akaunti ya Tegeta
ESCROW zilizolipwa kwa PAP ambayo si mmiliki halali wa IPTL.
Kwa maana hiyo fedha hizo zilitolewa kwa watu hao kama rushwa
na kuzitakatisha fedha hizo haramu. Aidha, kamati inapendekeza
kwamba Akaunti zote zilizohusika na miamala hii haramu ya
Akaunti ya Tegeta ESCROW, akaunti zao zifungwe (freeze) na 99
wenye akaunti hizo walazimishwe kurejesha fedha hizo kwa
mujibu wa Sheria (Anti Money Laundering) ikiwa ni pamoja na mali
zao kufilisiwa. Kwa upande wa viongozi wa Kisiasa wawajibike na
Watumishi wa umma wafukuzwe kazi.
3.2.4 Mheshimiwa Spika, Kamati imejiridhisha kwamba, suala la
akaunti ya Escrow ni jambo la utakatishaji wa fedha (Money
Laundering), kama alivyosema Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU
katika mahojiano yake na Kamati. Kamati inazitaka mamlaka
zinazohusika, ikiwemo Benki Kuu kuzitangaza benki za Stanbic na
Mkombozi Commercial Bank kama asasi za utakatishaji fedha
(Institutions of Money Laundering Concern).
3.2.5 Mheshimiwa Spika, Aidha, Kamati inalikumbusha Bunge lako
tukufu pendekezo muhimu lililotolewa na Kamati Teule ya
Mheshimiwa Dkt. Harrison Mwakyembe kuhusu sakata la maarufu
la Richmond. Kamati ilipendekeza:
“Mkataba kati ya TANESCO NA Richmond Development
Company LLC na sasa Dowans Holdings S.A. kama ilivyo
mikataba kati ya TANESCO na IPTL, SONGAS, AGGREKO 100
na Aistom Power Rentals inatoa unafuu usiostahili kwa
makampuni hayo ya umeme na kuiumiza TANESCO na
hatimaye watumiaji na walipa kodi kimapato, k.m.
mikataba hiyo kuwa na vipengele vya kuibana TANESCO
kuyalipa makampuni hayo kodi zinazohusika na
uendeshaji (operations) matengenezo/marekebisho ya
mara kwa mara ya mitambo (maintenance) gharama za
bima, ada za mawakili na washauri elekezi (consultants)
gharama za mafuta na gesi ya kuendeshea mitambo,
gharama za ukodishaji mitambo (capacity charges)
ambazo TANESCO hulipa kila mwezi si chini ya wastani
wa shilingi bilioni 2 kwa kila kampuni, izalishe au
isizalishe umeme. Kamati Teule inatoa rai kwa Serikali
kuwa mikataba yote hii ipitiwe upya mapema
iwezekanavyo kama ambavo mikataba ya madini
knavyopitiwa upya sasa na Serikali. Bila kufanya hivyo,
mzigo mkubwa wa gharama za umeme utawaelemea
wananchi na kushindwa kufikia azma ya Serikali ya
maisha bora kwa kila Mtanzania.”101
Mheshimiwa Spika, Kamati inapendekeza kwamba, azimio hili
litekelezwe kwa kupitia upya mikataba yote ya umeme ambayo
inalitafuna Taifa letu.
3.2.6 Mheshimiwa Spika, Kamati imejiridhisha kuwa Bodi ya Shirika la
Ugavi wa Umeme Nchini (TANESCO) bila sababu zozote za msingi
ilikataa mapendekezo ya Menejimenti ya Shirika ya kutoruhusu
uchotwaji wa fedha kutoka Benki Kuu akaunti ya Tegeta ESCROW
na hivyo kusababisha kulikosesha Shirika fedha zake inazohitaji
sana kutokana na hali mbaya ya Shirika. Ikumbukwe kuwa Shirika
la TANESCO lilipata hasara ya shilingi bilioni 467.7 katika mwaka
wa fedha unaoishia Desemba 31, 2013. Hasara hiyo imekuwa
ikiongezeka mwaka hata mwaka toka mwaka 2010 (bilioni 5),
2011 (bilioni 43), 2012 (bilioni 177) na hivyo hadi kufikia Desemba
31, 2013, jumla yote kuu ya hasara (accumulated loss) ilikuwa
imefikia shilingi trilioni 1.45.
Kamati pia imethibitisha kuwa Bodi ya TANESCO mpaka sasa
haijatekeleza hukumu ya ICSID 2 na kukokotoa upya viwango vya
malipo ya ‘capacity charges’ na hivyo kupelekea TANESCO na
Serikali kuendelea kuilipa IPTL/PAP kila mwezi shilingi Bilioni 4.5 102
($2.6m kila mwezi) izalishe au isizalishe umeme. Kamati inaitaka
Serikali kuvunja mara moja Bodi ya TANESCO na TAKUKURU
iwafungulie mashtaka ya matumizi mabaya ya ofisi wajumbe wote
waliohusika kupitisha maamuzi hayo ya kifisadi, ili iwe fundisho
kwa wajumbe wengine wa bodi za Mashirika ya Umma kwamba
watahukumiwa kwa maamuzi mabovu wanayoyafanya.
3.2.7 Mheshimiwa Spika, Kamati imethibitisha kuwa Katibu Mkuu wa
Wizara ya Nishati na Madini aliingia makubaliano ya kutoa fedha
katika Akaunti ya Tegeta ESCROW bila kujiridhisha kikamilifu kuwa
maamuzi ya hukumu ya ICSID 2 yalikuwa bado kutolewa na hivyo
kusababisha fedha kutolewa bila kukokotoa upya gharama za
‘capacity charges’, jambo ambalo limesababisha kupoteza fedha za
umma.
Vile vile, Kamati imebaini kuwa, Katibu Mkuu hakufanya uchunguzi
wa kina (due diligence) kujiridhisha uhalali wa Kampuni ya
Mechmar kuuzwa kwa Piperlink na baadaye kuuzwa kwa PAP, na
hivyo kusababisha fedha za akaunti ya Tegeta ESCROW kulipwa
kwa asiyestahili na kinyume cha Mkataba wa akaunti ya Escrow.
Kwa maana hiyo, Katibu Mkuu, Wizara ya Nishati na Madini, 103
pengine kwa uzembe wake ama kwa kukusudia kwa sababu
anazozijua yeye mwenyewe zaidi, amesaidia uchotwaji na
hatimaye utakatishaji wa fedha haramu.
Mheshimiwa Spika, Kamati pia imethibitisha uzembe wa hali ya
juu uliofanywa na Katibu Mkuu huyo, kushindwa kujiridhisha kama
masharti ya Sheria ya kodi ya Mapato Sura ya 333, Kifungu cha
90(2) yalitekelezwa. Kifungu hicho kimsingi kinaitaka mamlaka ya
‘approval’’ ya uhamishaji wa Makampuni kutotambua Kampuni
mpaka kwanza kodi za uhamishaji ziwe zimelipwa na hati za
malipo ya kodi zimetolewa na mamlaka ya kodi.
Mheshimiwa Spika, Kamati inapendekeza kuwa uteuzi wa Katibu
Mkuu huyu utenguliwe, na TAKUKURU wamfikishe mahakamani
mara moja, kwa kuikosesha Serikali Mapato, matumizi mabaya ya
ofisi na kusaidia utakatishaji wa fedha haramu.
3.2.8 Mheshimiwa Spika, Kamati imethibitisha kuwa Naibu Waziri wa
Nishati na Madini alisema uongo Bungeni kwa kutamka kauli
ambazo zilizokuwa na lengo la kupotosha umma kuhusu akaunti ya
Tegeta ESCROW ikiwemo kutoa kauli ambazo zingeweza 104
kusababisha Nchi kuingia kwenye mgogoro wa kidiplomasia na
nchi ya Uingereza.
Kamati inapendekeza kuwa Naibu Waziri wa Nishati na Madini
(Madini) achukuliwe hatua kali za kinidhamu ikiwemo kutenguliwa
uteuzi wake. Kamati pia inapendekeza kuwa Naibu Waziri huyu
afikishwe mbele ya Kamati ya Bunge ya Maadili ili aadhibiwe kama
Mbunge kwa kusema uwongo Bungeni ili liwe fundisho kwa
wabunge wengine kuhusiana na kauli wanazotoa ndani ya Bunge
lako tukufu.
3.2.9 Mheshimiwa Spika, Kamati imethibitisha kuwa Waziri wa Nishati
na Madini amekuwa, mara kwa mara, akilipotosha Bunge lako
tukufu na Taifa kwa ujumla kuhusiana na Fedha za Akaunti ya
Tegeta ESCROW kwamba ndani ya fedha hizo hakukuwa na fedha
za umma.
Mheshimiwa Spika, hata mtu wa kawaida angeweza kujua
kwamba washirika wa ‘Tegeta Escrow Account’ ni akina nani na
masharti ya kutoka kwa fedha hizo kwenye akaunti ni yapi kwa
mujibu wa Mkataba wa uendeshaji wa akaunti hiyo. 105
Hata hivyo, katika hali ya kushangaza, aidha kwa makusudi ama
kwa sababu anazozijua vizuri zaidi mwenyewe, Waziri wa Nishati
ananukuliwa kwenye kumbukumbu rasmi za Bunge, Kwa nguvu
kubwa na kwa kujiamini, akitetea uchotwaji wa fedha hizo
kinyume na masharti ya Mkataba wa Escrow.
Aidha, Kamati imebaini kuwa Waziri wa Nishati na Madini ndiye
alikuwa dalali mkuu aliyewakutanisha Bwana Harbinder Singh Sethi
na Bwana James Rugemalira, tena katika ofisi ya Umma; na
pengine hii ndiyo iliyokuwa sababu ya upotoshaji huu. Waziri wa
Nishati na Madini alifanya udalali huo akijua dhahiri kuwa Bwana
Sethi hana uhalali wa kisheria kufanya biashara kwa jina la IPTL.
Iwapo Waziri wa Nishati na Madini angetimiza wajibu wake
ipasavyo, Fedha za Tegeta ESCROW zisingelipwa kwa watu
wasiohusika, na Nchi ingeweza kuokoa mabilioni yaliyopotea kama
kodi za VAT, Capital Gain Tax na Ushuru wa Stempu ambazo ni
sawa na takribani shilingi bilioni 30. 106
Mheshimiwa Spika, Kamati inapendekeza kuwa Mamlaka yake
ya uteuzi itengue uteuzi wa Waziri wa Nishati na Madini kutokana
sababu hizo zilizoelezwa.
3.2.10 Mheshimiwa Spika, Kutokana na kukua na hivi sasa
kukomaa kwa vitendo haramu vya wizi wa fedha ama mali za
umma na kukua ama kukomaa kwa vitendo vya rushwa kubwa na
uhujumu uchumi, inapendekezwa kwamba Bunge lako Tukufu
liridhie kuitaka Serikali kuanzisha kitengo maalumu cha
kushughulikia rushwa kubwa (grand corruption) kitakachokuwa na
nguvu ya kuendesha mashtaka kwa uhuru kamili, na kwamba
Bunge lako Tukufu liridhie kuanzishwa kwa Mahakama Maalum ya
kushughulikia Rushwa kubwa itakayoshughulikia kesi za rushwa
zitakazokuwa zikipelekwa kwake na kitengo maalum cha
kushughulikia rushwa kubwa.
3.2.11 Mheshimiwa Spika, Kamati imethibitisha kuwa
Mwanasheria Mkuu wa Serikali alitoa ushauri ulioipotosha Benki
Kuu ya Tanzania kuhusiana na hukumu ya Jaji Utamwa J. Kwa
kutumia madaraka yake vibaya, Mwanasheria Mkuu wa Serikali
aliagiza kodi ya Serikali yenye thamani ya shilingi 21 bilioni isilipwe 107
na hivyo kuikosesha Serikali mapato adhimu. Mwanasheria Mkuu
wa Serikali kwa kujua na kwa makusudi alilipotosha Bunge na
Taifa kwamba mgogoro uliopelekea kufunguliwa kwa Akaunti ya
ESCROW ulikuwa ni mgogoro wa Wanahisa wa IPTL badala ya
mgogoro kati ya TANESCO na IPTL. Kamati inapendekeza kuwa
uteuzi wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali utenguliwe mara moja na
kisha afikishwe mahakamani kwa matumizi mabaya ya Ofisi
yaliyopelekea Serikali kupoteza mabilioni ya fedha.
3.2.12 Mheshimiwa Spika, Kwa upande wa Waziri Mkuu
kuhusiana na suala hili, Kamati iliipitia kwa umakini Katiba ya
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 iliyoainisha
Kazi na Mamlaka ya Waziri Mkuu na kubaini kuwa, kwa mujibu wa
Ibara ya 52 (1):
“Waziri Mkuu atakuwa na madaraka juu ya udhibiti,
usimamiaji, utekelezaji wa siku hata siku wa kazi na
shughuli za Serikali ya Jamhuri ya Muungano.”
Na, Ibara ya 52 (2), inayosema; 108
“Waziri Mkuu atakuwa kiongozi wa shughuli za Serikali
Bungeni.”
Kisha Kamati ikajiuliza maswali kadhaa. Kwa mfano katika kutaka
kubaini ukweli na kujiridhisha Kamati ilijiuliza maswali yafuatayo
kuhusu Waziri Mkuu:
(a) Je, Waziri Mkuu alikuwa anajua sakata la utoaji wa
fedha katika Akaunti ya Tegeta ESCROW?
(b) Je, Waziri Mkuu alitimiza wajibu wake kwa mujibu wa
Ibara ya 52(1)?
(c) Je, Waziri Mkuu wakati akitoa matamshi yake Bungeni
alikuwa akitimiza wajibu wake kwa mujibu wa Ibara ya
52 (2)?
(d) Je, nini maana, uzito na ukweli wa matamshi ya mara
kwa mara ya Waziri Mkuu ndani na nje ya Bunge
kuhusiana na suala hili?
(e) Je, Waziri Mkuu alitoa maamuzi au maelekezo yoyote
ya kuzuia jambo hili lisifanyike?109
Mheshimiwa Spika, Baada ya kupitia vielelezo vilivyomo kwenye
ripoti ya CAG, Kamati imejiridhisha pasipo mashaka kuwa, Waziri
Mkuu, alikuwa ana taarifa zote kuhusiana na mchakato mzima wa
kuchotwa fedha kutoka katika akaunti ya ESCROW.
Ushahidi ulioletwa na ofisi ya CAG kwenye Kamati unaonyesha
kuwa Waziri Mkuu alikuwa akipata taarifa za jambo hili. Na Kamati
imesikitishwa kuona kuwa Waziri Mkuu hakuchukua hatua zozote
kuzuia muamala huu usifanyike.
Mheshimiwa Spika, Kamati, kwa kuzingatia kielelezo namba 22,
inathibitisha bila shaka kwamba, Waziri Mkuu alikuwa analijua
jambo hili vizuri na kwamba aliridhia muamala huu ufanyike. Ndiyo
maana katika maelezo yake ya Bungeni mara kadhaa Waziri Mkuu
alithibitisha kuwa fedha za Escrow hazikuwa fedha za Umma.
Mheshimiwa Spika, Mwalimu Julius Nyerere katika kitabu chake
cha Uongozi Wetu na Hatma ya Tanzania aliandika:
“…kubadili Waziri Mkuu sio jambo la ajabu. Ndugu
Rashid Mfaume Kawawa alikuwa Waziri Mkuu wangu 110
kwa muda mrefu. Hakuwa amefanya kosa lolote; lakini
nilitaka kumbadili na kuteua Waziri Mkuu mwingine.
Nilimwita, nikamwambia hivyo. Tukakaa pamoja mimi
na yeye, tukashauriana na kukubaliana nani anafaa
kushika nafasi yake. Nikamteua Hayati Edward Moringe
Sokoine. Najua kuwa watu wa aina ya Rashidi Kawawa
ni adimu sana Duniani, hawazaliwi kila siku; hata hivyo
ni jambo la kushangaza kidogo kwamba viongozi wetu
wa Mageuzi, hata bado hatujafa, wanaona kuwa ni
kosa kuwakumbusha kuwa vyeo walivyonavyo ni
dhamana. Wanadhani kuwa Uwaziri ni Usultani;
ukishakuwa Sultani utakufa sultani! Nadhani
wanakosea. Nchi hii imewahi kung’oa Masultani wa kila
aina. Tukianza kuvumilia Masultani wa kuchaguliwa,
tutapanda mbegu ya Masultani wa kuzaliwa. Narudia;
kumbadili Waziri Mkuu sio jambo la ajabu. Anaweza
kujiuzulu, anaweza kufukuzwa Nchi isitikisike. Lakini
huwezi kumtimua Rais wa Nchi bila kuitikisa Nchi
yenyewe. Ni vizuri jambo hili likatamkwa waziwazi na
likaeleweka sawasawa. Maana watu wengine
wananong’ona nong’ona kuwajibika kwa Rais kana 111
kwamba ni jambo la mchezo mchezo tu. Kulazimika
kumchukulia hatua Rais wa nchi ni mkasa na balaa kwa
Nchi yeyote ile.”
Mwisho wa kunukuu.
Mheshimiwa Spika, ni dhahiri kwamba viongozi wenye mamlaka
makubwa wanapaswa kila wakati kukumbuka kauli ya muasisi wa
Mapinduzi ya Zanzibar na Muasisi wa Muungano, Sheikh Thabit
Kombo, ambaye alikuwa akipenda kusema ‘weka akiba ya
maneno’.
Ni wazi kwamba maneno ya Waziri Mkuu hapa Bungeni
yaliuaminisha umma kuwa fedha zile siyo fedha za umma kiasi
kwamba gazeti la Serikali la Daily News la tarehe 1 mwezi Mei,
2014, likachapisha habari yenye kichwa kikubwa cha habari ‘IPTL
clean Deal – Pinda’. Na ofisi ya Waziri Mkuu haikukanusha.
Mheshimiwa Spika, ni jambo la kushangaza kuona kwamba,
jambo kubwa na zito kama hili lingeweza kufanyika bila ya
mamlaka za juu, hususan Mhe. Waziri Mkuu kufahamu. 112
Mheshimiwa Spika, kwa uzito na unyeti wa jambo hili, kwa
vyovyote vile, Waziri Mkuu anapaswa kuwajibika kwa kauli zake na
kwa kutokutekeleza wajibu wake wa kikatiba ipasavyo, ili
kurejesha imani ya wananchi kwa serikali yao na viongozi wao wa
kisiasa.
3.0 HITIMISHO
Mhesimiwa Spika, napenda kukushukuru sana kwa kuiamini
Kamati yetu kwa kuikabidhi jukumu hili nyeti. Nakuhakikishia
kwamba kazi hii imetekelezwa kwa haki iliyojengwa katika msingi
wa Taarifa ya Ukaguzi Maalum wa Ofisi ya Mdhibiti na Mkaguzi
Mkuu wa Hesabu za Serikali, na vyanzo vingine muhimu
vikijumuisha maelezo ya Ofisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa
(TAKUKURU) na Mamlaka ya Mapato nchini (TRA).
Mheshimiwa Spika, Kamati inatoa shukrani za dhati kwa vyombo
vya habari kwa kuwapasha habari Watanzania kuhusiana na suala
hili. Kwa namna ya pekee kabisa Kamati inalipongeza gazeti la
The Citizen kwa msimamo wake thabiti bila kujali vitisho.113
Mheshimiwa Spika, Kamati yetu inayo imani na Bunge Lako
Tukufu kwamba litaitumia Taarifa hii ipasavyo katika kutekeleza
Wajibu wake wa kuisimamia na kuishauri Serikali itekeleze wajibu
wake katika misingi ya haki, uadilifu, uzalendo, usawa, uwazi na
uwajibikaji. Tunawashukuru sana Waheshimiwa Wabunge wote
kwani katika kipindi chote cha kuandika Taarifa hii mlitutia moyo
kwa kuonesha dhahiri kwamba mnaihitaji Taarifa yetu ijadiliwe
Bungeni.
Mheshimiwa Spika, naomba pia kuishukuru Ofisi ya Spika kwa
maelekezo thabiti ya namna ya kutekeleza jukumu hili.
Naomba pia kumshukuru Katibu wa Bunge, Dkt. Thomas D.
Kashillilah na Wajumbe wa Sekretarieti yake kwa ushauri makini
katika kipindi chote ambacho Kamati ilikuwa ikitekeleza jukumu
hili. Kipekee nawashukuru pia Kaimu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu
wa Hesabu za Serikali, Ndg. Francis Mwakapalila, Mkurugenzi
Mkuu wa Ofisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa, Dkt. Edward
Hoseah na Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato nchini, Bw.
Rished Bade kwa ushirikiano walioipatia Kamati.114
Mwisho, nawashukuru Watumishi wote wa Bunge na vyombo
vingine vya kiusalama vilivyohusika katika kuisaidia Kamati
kutekeleza jukumu lake.
Mheshimiwa Spika, naomba Bunge lako tukufu lipokee Taarifa
hii, lijadili na kupitisha mapendekezo yote tuliyoyatoa kuwasilisha.
Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja.
Zitto Zuberi Kabwe, Mb.
MWENYEKITI
KAMATI YA BUNGE YA HESABU ZA SERIKALI (PAC)
26 NOVEMBA, 2014

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527