Maskini!! MWINJILISTI AUAWA AKIMFANYIA MAOMBI MGONJWA



Kamanda wa polisi mkoa wa Mbeya Ahmed Msangi
MTU mmoja aliyehamamika kwa jina la AMBUMBULWISYE MWASOMOLA (35), ambaye ni muinjilisti na mkazi wa Kijiji cha Lukasi, ameuawa kwa kupigwa kichwani na mchi wa kutwangia.



Aliyefanya mauaji hayo amefahamika kwa jina la SWALAPO MWAISANILA (56), mkazi wa Kijiji cha Lwangwa ambaye ni mgonjwa wa akili. 



Tukio hilo lilitokea juzi TAREHE 27.09.2014 Majira ya SAA 23:30 USIKU, huko katika kijiji cha Luka, Kata ya Lwangwa, tarafa ya Busokelo, wilaya ya Rungwe mkoani Mbeya.



Mauaji hayo yalitokea baada ya Muinjilisti huyo wa kanisa la Baptisti kutaka kumfanyia maombi mtuhumiwa huyo kutokana na ugonjwa wa akili alio nao mtuhumiwa, ndipo mtuhumiwa alichukua mchi na kumpiga nao marehemu kichwani na kupelekea kifo chake.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527