Kimenuka!! SASA DEREVA UKIONGEA NA SIMU UNAFUTIWA LESENI YAKO,TENA SASA KUPIMWA AFYA ZAO



Jeshi la Polisi kikosi cha usalama Barabarani kwa kushirikiana na Mamlaka ya usafiri wa Nchi kavu na Majini SUMATRA limeanzisha mkakati wa kuwafungia leseni madereva watakaobanika kuendesha magari huku wakiwa wanazungumza na simu za mkononi.
zoezi hilo limekuja kufuatia kile kinachodaiwa kuwepo kwa ongezeko la ajali za barabarani ambazo zinasababishwa na uzembe ambao unasababishwa na unywaji wa pombe,kuchoka na kuzungumza na simu hizo.

  
Takwimu zinaonyesha kuwa kumekuwa na ongezeko la matukio 264 ya ajali barabarani kwa mwaka 2013 sawa na asilimia 1.1 tofauti na mwaka 2012 ambapo matukio yalikuwa 23,578.
  
Kwa mwaka huu kati ya januari hadi June idadi ya ajali zilizoripotiwa zilikiwa 8,405 zilizosababisha vifo 1743 na majeruhi 7,523 hali ambayo Kamanda Mpinga anasema ipo mikakati mbadala ya kukabiliana na hali hiyo.

Inatajwa kuwa madereva wengi hawana tabia ya kupima afya zao mara kwa mara,inaelezwa kuwa magonjwa ya macho,kisukari pamoja na shinikizo la damu pia linachangia ajali nyingi.
  
Kampuni ya Bia Tanzania TBL itatumia shilingi milioni 800 katika kufanikisha zoezi la kupima afya za madereva katika vituo vitatu vya afya vya Msata Mkoani Pwani,Mikese Mkoani Morogoro pamoja na Makuyuni Mkoani Arusha lengo likiwa ni kuepukana na ajali hizo.

BONYEZA HAYA MANENO "U LIKE PAGE YETU"TUKUTUMIE HABARI ZETU MARA TU ZINAPOTOKEA

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post