Mdhamini wa shindano la Miss Lake zone 2014 LEONARD BUGOMOLA, mkazi wa Mtaa wa Nyamalembo Wilayani Geita Mkoani hapa ambaye ni Mkurugenzi wa Lenny Hotel, akiwa na Walimbwende 18 akiwaonyesha gari alilotoa zawadi kwa ajili ya mshindi wa kwanza atakayeibuka kidedea mwishoni mwa mwezi huu. Picha na Valence Robert-Malunde1 blog Geita
Nani kuondoka na gari hilo kati ya warembo 18 kutoka kanda ya ziwa . Picha na Valence Robert-Malunde1 blog Geita
IKIWA ni siku chache wasichana 18 kutoka Mikoa ya Kanda ya Ziwa wanaoshiriki mashindano ya Taji la Miss Lake Zone mwaka 2014 kutembelea kituo cha watoto yatima cha Moyo wa Huruma kilichopo mtaa wa Mbugani Wilayani Geita mkoani Geita na kutoa misaada mbalimbali yenye thamani ya shilingi laki 350,000/= Mamiss wameendelea kuonekana mfano kwa kufanya usafi katika mji wa Geita.
Wakizungumza na Malunde1 blog Mamiss hao walisema kuwa wameamua kufanya usafi katika mji huo ikiwa ni kutekeleza agizo la Mkuu wa Wilaya hiyo Omary Mangochie ya kufanya mji kuwa msafi kwa kufanya usafi kila Alhamis .
Mamiss hao wametoa shukrani zao kubwa kwa mdhamini wao Leonard Bugomola ambaye ametoa vyumba 10 vya kulala ambapo kila chumba ni shilingi 80,000/= kila siku na chakula chenye thamani Tsh 15,000 kwa kila mshiriki huku wakiishi hotelini kwake kwa siku kumi wakiwa kwenye mazoezi.
Katika namna ya pekee pia ametoa gari lenye thamani ya Tshs. Milioni kumi (10,000,000/=) kwa atakaye kuwa mshindi wa kwanza katika shindano la Miss Lake zone 2014.
Mdhamini huyo Leonad Bugomola ambaye ni mfanya bishara mkoani humo pia mmiliki wa Lenny Hotel alisema kuwa ameamua kutoa zawadi hizo kutokana na Mungu kumjalia alivyo navyo na kuwa na kipaji cha kupenda michezo mbalimbali.
Bugomola aliwaomba wafanya biashara wenzake wa mkoa wa Geita kujitolea kwa kudhamini Mamiss na kuacha Dhana ya kuwa Umiss ni uhuni kwani Umiss ni ajira kama ajira zingine.
Shindano la kumpata Miss ake Zone litafikia tamati mwishoni mwa mwezi huu wa nane (8) mbapo mshindi wa kwanza atajinyakulia zawadi ya Gari.
Na Valence Robert-Malunde1 blog-Geita
TAFADHALI BOFYA HAPA U LIKE PAGE YETU TUKUTUMIE "HABARI" MOJA KWA MOJA KILA ZINAPOTOKEA
TAFADHALI BOFYA HAPA U LIKE PAGE YETU TUKUTUMIE "HABARI" MOJA KWA MOJA KILA ZINAPOTOKEA