MADUKA YA WALIOJIUNGANISHIA UMEME KINYEMELA YATEKETEA KWA MOTO HUKO GEITA

MADUKA  wawili ya wafanyabiashara wa katika mji mdogo wa Buseresere katika wilaya  ya Chato mkoani Geita yameteketea kwa moto na kuunguza mali ambayo inadaiwa kuwa ni zaidi ya shilingi milioni mia moja.

Tukio hilo limetokea usiku wa kuamkia jana majira ya saa 10 na nusu usiku katika mtaa wa msikitini na kuteketeza mali za wafanya biashara wawili.
 
Katika tukio hilo familia moja ya Yahaya Runwa imenusurika kuteketea kwa moto huo.

Runwa alieleza kuwa  usiku alisikia mlipuko mkubwa nje kwenye vibanda vya biashara alivyowapangisha  wafanyabiashara hao na alipotoka nje alikuta mtungi wa gesi umelipuka na unawaka moto na aliporudu ndani hari ilikuwa mbaya zaidi ndipo akaanza kupiga kelele za kuomba msaada kwa wananchi.

Akizungumza na waandishi wa habari afisa mtendaji wa kata hiyo Daudi Ruhangija alisema chanzo cha moto huo  kuwa ni hitilafu ya umeme uliokuwa umeunganishwa kinyemela katika nyumba hiyo.

Ruhangija aliwataja waathirika hao kuwa ni Faridu Abdul ambaye  ni mfanya biashara wa sipea za magari na pikipiki  na mwingine ni Maiko Hamko ambaye ni mfanya biashara wa mitungi ya gesi na wote ni wakazi wa mji huo.

Kaimu kamanda wa zima moto mkoani hapa Hamidu Ngiya alisema  baada ya kupata taarifa kuhusu tukio hilo kutoka kwa afisa mtendaji wa kata walifika kwenye eneo la tukio wakiwa na gari lenye namba FT3HGA10034 na kufanikiwa kuzima moto kwa kushirikiana na wananchi waliowakuta kwenye eneo la tukio.

Hata hivyo baadhi ya changamoto alizoelezea Hamidu katika kutekeleza zoezi hilo ni pamoja na uhaba wa vitendea kazi ikiwemo gari moja mkoa mzima,umbali wa maji ya kuzimia,na uchache wa wafanyakazi ambapo wapo wanane wakati,vilevile ukosefu wa unifomu wanapokuwa kazini ili waweze kutambulika kwa urahisi.

Aidha aliwataka wananchi waache tabia ya kujiunganishia umeme kwa njia ambazo siyo rasmi kwani kwa kufanya hivyo itakuwa ni kuhatarisha maisha ya wananchi.

Na Valence Robert-malunde1 blog- Geita

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527