Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MAADHIMISHO YA SIKU YA MTOTO WA AFRIKA YAISHIA MAKABURINI SHINYANGA,YALIANZA KWA MAANDAMANO.TAZAMA PICHA

Ni katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika ambayo huadhimishwa kila mwaka Juni 16,katika kusherehekea siku hiyo muhimu kuwakumbuka watoto waliopoteza maisha kule nchini Afrika kusini wakidai haki zao.Katika kuadhimisha siku hiyo muhimu manispaa ya Shinyanga ilifanya maandamano yaliyoanzia katika uwanja wa shule ya sekondari Buluba na kuelekea kupitai maeneo mbalimbali mjini Shinyanga na kuishia katika shule ya msingi Mapinduzi A,ambako kulifanyika mkutano,maonesho mbalimbali zikiwemo shughuli zinazofanywa na watoto baadaye wadau wa haki za watoto waliekea katika makaburi ya Majengo mjini Shinyanga na kufanya misa ya kumkumbuka mtoto Rose Dotto Peter(12) aliyeuawa kikatili kisha mwili wake ukiwa kwenye boksi  kutupwa kwenye jalala la takataka katika eneo la Ngokolo mjini Shinyanga siku ya mtoto wa Afrika mwaka 2013

Maandamano yanaendelea watoto wa shule za msingi,sekondari,taasisi,asasi na wadau mbalimbali wa haki za watoto wakiwemo waandishi wa habari walikuwepo

Wakati wa maandamano

Watoto wakiimba kwaya katika viwanja vya shule ya msingi Mapinduzi A muda mfupi baada ya  mgeni rasmi naibu meya wa manispaa ya Shinyanga ndugu David Nkulila kupokea maandamano hayo

Mgeni rasmi naibu meya wa manispaa ya Shinyanga ndugu David Nkulila(mwenye kofia kushoto) akikagua vibanda vya maonesho katika viwanja vya Shule ya msingi Mapinduzi.Hapa ni katika banda la AMREF Kulia ni bwana Gaspar Misungwi ambaye ni afisa mradi wa Tubadilike afya ya uzazi kutoka AMREF akitoa maelezo kwa mgeni rasmi kuhusu shughuli wanazozifanya kuhusiana na watoto katika jamii
Watoto wakionesha shughuli wanazofundishwa na shirika la Compassion kwa mgeni rasmi 

Mkurugenzi wa Compassion kituo cha AICT Ngokolo bwana Peter Joshua akimwongoza mgeni rasmi David Nkulila ambapo alisema compassion inafundisha pia watoto kuhusu namna na kutumia vyombo vya muziki kama unavyoona pichani mtoto anacheza na vyombo utafikiri alizaliwa navyo

Watoto wakicheza katika viwanja vya shule ya msingi Mapinduzi A mjini Shinyanga

Wadau wa haki za watoto wakifuatilia kilichokuwa kinajiri uwanjani hapo

Mwenyekiti wa baraz la watoto katika kata ya Ngokolo  Anitha Joseph ambaye pia ni mwanafunzi wa shule ya msingi Mapinduzi A katika manispaa ya Shinyanga wakati akisoma risala kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika shule ya Mapinduzi A katika manispaa hiyo.

Wadau wa haki za watoto wakisikiliza risala ya watoto

Watoto wakifanya yao katika viwanja vya shule ya msingi mapinduzi A jana mjini Shinyanga

Wadau wa haki za watoto wakiwa katika makaburi ya Majengo mjini Shinyanga ambako kulifanyika misa ya kumwombea mtoto Rose Dotto Peter (12) aliyeuawa kikatili mwaka jana na kuzikwa katika makaburi hayo huku manispaa ya Shinyanga ikichukua jukumu la kujenga kaburi la mtoto huyo kama kumbukumbu.Misa ya kumwombea mtoto Rosemary imeongozwa na wakili paroko kanisa katoliki parokia ya Shinyanga mjini jimbo la Shinyanga padre Joseph Okuruti.

wakili paroko kanisa katoliki parokia ya Shinyanga mjini jimbo la Shinyanga padre Joseph Okuruti akibariki kaburi la mtoto Rose aliyeuawa mwaka 2013 siku ya mtoto wa Afrika

Kaburi la mtoto Rose Dotto aliyeuawa kikatili kwa kupigwa kitu kizito kichwani kisha mwili wake kutupwa jalalani siku ya mtoto wa Afrika mwaka 2013

Mgeni rasmi katika maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika katika manispaa ya Shinyanga David Nkulila akizungumza baada ya misa ya kumwombea mtoto Rose Dotto aliyeuawa kikatili mwaka 2013-Picha zote na Kadama Malunde wa Malunde1 blog

Soma hapa chini Habari kamili---

Watoto katika manispaa ya Shinyanga wameiomba serikali kutoa elimu ya kutosha inayohusu sera na haki za watoto ili watoto waweze kutambua haki zao za msingi katika kukabiliana na changamoto zinazowakabili ikiwemo ukatili na unyanyasaji.

Wito huo umetolewa jana na mwenyekiti wa baraz la watoto katika kata ya Ngokolo  Anitha Joseph ambaye pia ni mwanafunzi wa shule ya msingi Mapinduzi A katika manispaa ya Shinyanga wakati akisoma risala kwenye maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika yaliyofanyika katika shule ya Mapinduzi A katika manispaa hiyo.

Akisoma risala hiyo alisema matukio ya unyanyasaji na ukatili dhidi ya watoto unachangiwa na watoto kutojua haki zao huku jamii nayo ikiwa haielewi chochote matokeo yake kila kukicha ukatili,unyanyasaji unazidi kujitokeza katika jamii.

“Tunaiomba serikali na wadau mbalimbali kutoa elimu ya kutosha inayohusu sera na haki za mtoto kwa jamii yetu na wakazi wa manispaa ya Shinyanga,kwani tunanyanyasika,pia tunaiomba serikali yetu iwachukulie hatua wote wanaokiuka na kuvunja upatikanaji wa haki ya mtoto kupata elimu bora”,alisema Anitha.

Katika hatua nyingine mwenyekiti huyo wa watoto alisema miongoni mwa vikwazo katika sekta ya elimu ni pamoja na jamii kuwa na uelewa mdogo kuhusu elimu hali inayosababisha watoto kukosa elimu bora kutokana na vikwazo wanavyovipata mfano baadhi ya jamii kuwanyanyasa watoto wa kike kwa kuozesha katika umri mdogo badala ya kuwasomesha.

Akizungumza katika maadhimisho hayo mgeni rasmi naibu meya wa manispaa ya Shinyanga David Nkulila alisema manispaa ya Shinyanga bado inakabiliwa na ukatili dhidi ya watoto na sasa limezuka wimbi la wazazi na walezi kukwepa kulea watoto kwa visingizio mbalimbali kama vile kudai kuwa wana hali ngumu kimaisha.

Nkulila alisema wazazi na walezi wamekuwa wakikwepa kulea watoto na kuanza kuilalamikia serikali iwatendee haki wakati wanakwepa majukumu yao kama walezi wa watoto.

Maadhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika katika manispaa ya Shinyanga yameanza kwa maandamano kisha misa ya kumwombea mtoto Rosemary Dotto Peter(12) aliyeuawa kikatili kwa kupigwa kitu kizito kichwani kisha mwili wake kufungwa kwenye boksi kisha kutupwa kwenye jalala la takataka eneo la Ngokolo mjini Shinyanga mwaka 2013 siku ya mtoto wa Afrika.

Misa ya kumwombea mtoto Rosemary imefanyika katika makaburi ya Majengo mjini Shinyanga alikozikwa na kaburi lake kujengwa na manispaa ya Shinyanga kama kumbukumbu,ambapo misa hiyo imeongozwa na wakili paroko kanisa katoliki parokia ya Shinyanga mjini jimbo la Shinyanga padre Joseph Okuruti.

Na Kadama Malunde- Shinyanga

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com