Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

KUMBE WAZIRI KAWAMBWA KAZUSHIWA KIFO,UKWELI NI KWAMBA HAJAFARIKI DUNIA

  • Kuna habari imetapakaa katika mitandao ya kijamii kuwa waziri wa Elimu na mafunzo ya ufundi wa Tanzania mh. Shukuru Kawambwa amefariki dunia.... 

    Huu hapa ndiyo ukweli wa habari hii,kama mtandao huu wa Malunde1 blog ulivyoahidi kukutaarifu kuhusu ukweli wa habari hiyo,ambayo kiukweli malunde1 blog ilipokea taarifa hizo kwa masikitiko makubwa.

  • Yohana Mwambene
    Yohana Mwambene


    Necta shared a Timeline. 4 hours ago Habari hii ya kifo tulipewa na ndugu watatu ambao ni https://www.facebook.com/deus.nyongole na mwengine ni https://www.facebook.com/marco.wawa na watatu wao ni https://www.facebook.com/france.ignas tunasikitika kuwambia ya kwamba habari hiyo ilikuwa ya uongo na wahusika wanatiwa mbaroni kwa usaili zaidi.
TAARIFA YA KANUSHO HII HAPA


Ndg Watanzania,WanaBagamoyo na wapenda maendeleo, kwa niaba ya CCM-Bagamoyo na Ofisi ya Mbunge-Jimbo la Bagamoyo napenda kuleta kwenu Masikitiko yetu kwa niaba ya Chama na Familia ya Mheshimiwa Mbunge Shukuru Jumanne Kawambwa kutokana na Usumbufu ambao umesababishwa na habari zinazoenezwa Mitandaoni kwamba Mheshimiwa Kawambwa amekumbwa na Umauti akiwa njiani anaelekea Mwanza.

UKWELI
Mheshimiwa Shukuru Jumanne Kawambwa yupo Nchini Canada Akitimiza majukumu yake. Hivyo Watanzania na wana Bagamoyo mnaombwa radhi kwa usumbufu uliotokea na kwamba Mheshimiwa Mbunge yuko na Afya njema na utekelezaji wa Majukumu unaendelea kama kawaida.
 

 Ndg.Ridhiwani Kikwete (Mnec)
Mbunge -Chalinze 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com