ASKARI POLISI AGONGWA GARI NA KUFARIKI PAPO HAPO WAKATI AKISAFIRI KWA BAISKELI MAARUFU DALADALA -SHINYANGA





Mkuu wa jeshi la polisi nchini IGP Said Mwema


Jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga na taifa kwa ujumla limepata msiba kufuatia kifo cha askari polisi   Rehema  James (30) kufariki dunia papo hapo hapo jana jioni  baada ya kugongwa na gari   katika eneo la Kambarage mjini Shinyanga akiwa amepakizwa kwenye baiskeli maarufu daladala hapa mkoani Shinyanga.
 
Akizungumza na malunde1.blogspot.com, Kaimu kamanda wa polisi mkoa wa Shinyanga  ACP Kihenya Kihenya amesema askari aliyefariki dunia ni WP 5090, PC Rehema James Mniko.
 
Amesema askari huyo akiwa amepakizwa kwenye baiskeli maarufu kama daladala ghafla aligongwa na gari aina ya scania lenye namba za usajili  BLQ 546 na kufariki dunia papo hapo wakati mwendesha  baiskeli akijaribu kulipita gari hilo wakati likikata kona .
Amesema tayari mwili wa marehemu umesafirishwa kwenda nyumbani kwao Kitunda jijini Dar es salaam kwa ajili ya mazishi yanayotarajiwa kufanyika kesho jumapili.
 
    Chanzo cha ajali hiyo bado kinachunguzwa na jeshi la polisi.

MUNGU AILAZE MAHALI PEMA PEPONI ROHO YA MAREHEMU ASKARI REHEMA. AMINA!

 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post