MGEJA ASEMA TUSIWE NA SHUKRANI YA PUNDA

Wanachama wa CCM wakifuatilia hotuba ya mwanyekiti wa CCM mkoa wa Shinyanga Hamis Mgeja
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi CCM mkoa wa Shinyanga ndugu Hamis Mgeja amewataka wananchi  kuacha kubeza mafanikio yaliyofikiwa na serikali ya CCM  tangu iingie madarakani mwaka 2010, na kuongeza kuwa hakuna serikali yoyote duniani isiyokuwa na matataizo na njia pekee ya kuondoa matatizo ni kufanya kazi kwa juhudi na maarifa wala siyo kukikimbia chama.

Mgeja ameyasema hayo jana katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika eneo la Ngokolo Mitumbani Mjini Shinyanga wakati wa ziara yake kuangalia utekelezaji wa ilani ya CCM  tangu iingie madarakani mwaka 2010 ambapo alisema mambo kadha wa kadha yamefanywa na chama hicho ikiwemo masuala ya elimu,barabara,maji na  afya na kutoyaona mafanikio yaliyofikiwa akalinganisha  na shukrani ya punda kuwa  ni mateke.

Amesema mkoa wa Shinyanga hivi sasa una mabadiliko makubwa kwani wananchi wanapata maji safi na salama kutoka ziwa Victoria huku viwanda mbalimbali vikiendelea kujengwa hali ambayo itasaidia vijana wengi kupata ajira.

Aidha amewataka wananchi kuwapuuza wapinzani wanaohubiri kuhusu maandamano ama nguvu ya umma na kusisitiza kuwa hakuna serikali yoyote duniani iliyoingia kwa njia ya nguvu ya umma imefanikiwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم