TANZANIA,UNESCO KUDUMISHA USHIRIKIANO SEKTA YA MAJI

  




Na Mwandishi Wetu,UNESCO- NEW YORK

Waziri wa Maji Mhe Jumaa Aweso amekutana na Naibu Mkurugenzi mkuu wa shirika la Umoja wa Mataifa UNESCO Bwana Xing Qu ofisi za UNESCO New York kwa lengo la kujadiliana juu ya mahusiano na mashairikiano katika usimamizi wa uendelezani wa Rasilimali za Maji na ushirikiano katika usimamizi wa Maji Shirikishi.

Waziri Aweso amewasilisha ombi la Tanzania kujengewa uwezo na UNESCO katika usimamizi na uendelezaji wa Rasilimali za Maji na utekelezaji wa miradi ya Maji, uandaaji wa maandiko ya Miradi na utafutaji wa fedha.


Aidha; Naye Naibu Mkurugenzi mkuu UNESCO Mr Xing Qu ameahidi ushirikiano katika maeneo ya kipaumbele kwa Afrika ikiwemo usimamizi wa Maji chini ya Ardhi, kujenga uwezo wa taasisi katika tathmini ya usimamizi wa Rasilimali za Maji.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments