WANAFUNZI WANNE PEKEE KATI YA 88 WARIPOTI KIDATO CHA KWANZA


Wanafunzi wanne kati ya 88 waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika shule ya Sekondari Izumachel iliyopo wilayani Geita

Ikiwa wiki moja imepita tangu kuanza kwa msimu wa masomo mwaka 2023 Tanzania, wanafunzi wanne kati ya wanafunzi 88 waliochaguliwa kujiunga kidato cha kwanza katika shule ya sekondari Izumachel iliyopo wilayani Geita mkoani hapo ndio walioripoti katika shule hiyo.

Shule hiyo iliyoanza mwaka 2022 ikiwa na wanafunzi 40 wa kidato cha pili hadi sasa walioripoti na kuanza masomo ni wanafunzi 26 na kufanya shule nzima kuwa na wanafunzi 30 kati ya 128 walioachaguliwa kujiunga na shule hiyo.


chanzo Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments