YANGA SC YAIADHIBU DODOMA JIJI 2-0, MAYELE ATUPIA MBILI


*********************

NA EMMANUEL MBATILO


FISTON Kalala Mayele amendelea kutikisa nyavu ndani ya ligi kuu NBC baada ya leo kupachika mbao mawili na kuisaidia timu yake kuondoka na ushindi wa mabao mawili dhidi ya Dodoma Jiji.

Mchezo huo ambao ulichezwa kwenye dimba la Liti mkoani Singida tumeshuhudia wachezaji wengi wa Yanga kupata majeruhi kwenye mchezo huo akiwemo nahodha wao Bakari Nondo Mamnyeto na Feisal Salum.


Kipindi cha kwanza Yanga Sc ilikuwa mbele kwa bao 1-0, bao ambalo lilifungwa kabla ya kwenda mapumziko dakika ya 43 ya mchezo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments