Familia moja kutoka kijiji cha Bomeroka huko Kitutu Chache kaunti ya Kisii nchini Kenya inaomboleza ajuza aliyeuawa na mwanawe.
Jamaa huyo mwenye umri wa miaka 34, anayesemekana kuwa mraibu wa dawa za kulevya, aliripotiwa kupandwa na mori baada ya kuhisi kuwa kiasi cha chakula alichotengwa kilikuwa kidogo.
Kulingana na mfanyakazi wa shambani wa nyumba hiyo, mshukiwa alitaka kula chakula chote cha mchana ambacho kilikuwa kimetayarishwa kwa ajili ya familia nzima.
Marehemu alipomsihi asichukue chakula chote, alinyakua panga na kumrukia mara moja akamkata mkono.
“Alitaka kuchukua chakula chote mamake alipomtaka awafikirie ndugu zake ambao walikuwa bado hawajala, alipandwa na mori na hapo mara moja akamjeruhi vibaya kwa panga,” alisema mfanyakazi huyo.
Mwanamke huyo alikata roho kutokana na kuvuja damu nyingi akikimbizwa hospitalini.
Chanzo: TUKO.co.ke
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin