MAJARIBIO YA CHANJO YA EBOLA KUFANYIKA UGANDA


Zaidi ya dozi 20,000 za chanjo ya majaribio dhidi ya ugonjwa wa Ebola aina ya Sudan ambao umeikumba nchi ya Uganda zinatengenezwa nchini india.

Taarifa zinasema kwamba chanjo hizo zinaweza kutengenezwa na Taasisi ya Serum ya India na kutumika katika majaribio kuona kama zinaweza kufanya kazi ya kukabiliana na mlipuko wa sasa nchini Uganda.

Chanjo kadhaa zimetumwa huko Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo dhidi ya aina ya hiyo ya Ebola, lakini hakuna chanjo iliyothibitishwa yenye ufanisi dhidi ya aina ya Sudan.

Watu 19 wamefariki kufikia sasa na kumekuwa na visa 54 vilivyorekodiwa tangu kuzuka kwa janga hilo mwezi uliopita.

Mwishoni mwa wiki, Rais Yoweri Museveni aliweka aliziweka karantini wilaya mbili

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments