ZAIDI YA WATU 1000 KUHUDHURIA KONGAMANO LA UWEZESHAJI

  



Mkuu wa  Mkoa wa Dodoma Rosemary Senyamule.,

 

Na Dotto Kwilasa
 DODOMA.

WAZIRI Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania,Kassim Majaliwa anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Kongamano la sita la uwezeshaji Wananchi kiuchumi ambalo litafanyika Septemba 19 Mwaka huu Jijini Dodoma.

Mkuu wa Mkoa wa Dodoma,Rosemary Senyamule  ameyaeleza hayo jana Jijini Dodoma wakati akizungumza na Waandishi wa Habari kuhusiana na Kongamano hilo ambalo litahudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali pamoja na wadau wa maendeleo.

Aidha Mkuu huyo wa Mkoa wa Dodoma ametoa Wito kwa wakazi wa Dodoma kuchangamkia fursa kupitia Kongamano hilo ikiwa ni pamoja na kuandaa miundombinu mbali mbali ya kiuchumi ikiwemo biashara ya chakula na malazi.

Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza hilo,Beng' Issa akaeleza lengo la Kongamano hilo kuwa ni fursa 
katika kuwawezesha wananchi kiuchumi kwa ustawi wa taifa kwa ujumla.

Amesema  jukwaa hilo litahudhuriwa na zaidi ya watu1000 kwa kuhusisha jopo la majadiliano la wakuu wa Mikoa pamoja na Wataalam kuhusiana na masuala yakuwawezesha wananchi kiuchumi.

Naye Meneja wa Benki ya Stanbic Tawi la Dodoma Opi Ligolola ametumia nafasi hiyo kuipongeza Serikali kutokana na jitihada zake katika kuwawezesha wanachi kiuchumi na kueleza Mkataba walioingia na Baraza la uwezeshaji Wananchi kiuchumi,

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments