JAMBO ATUA DODOMA KUNUNUA ZABIBU

Kampuni ya Jambo Food Products ya Mjini Shinyanga jana imeanza kununua zabibu kutoka kwa wakulima katika maeneo mbalimbali mkoani Dodoma ikiwa ni siku chache baada ya tamko la Waziri wa Kilimo Mh. Hussein Mohamed Bashe alililotoa wakati akijibu changamoto za wakulima wa zabibu walizowasilisha mbele ya Mh. Rais Samia Suluhu Hassan aliposimama kuwasilimia eneo la Mpunguzi,Jijini Dodoma.


Mwakilishi wa Kampuni ya Jambo Ndg. Emmanuel Ngusa amewahakikishia wakulima wa zabibu wa Mkoani Dodoma juu ya nia na dhamira ya Kampuni ya Jambo kuendelea kuwa soko la uhakika la zabibu baada kujiridhisha ubora.


Zoezi la ununuaji wa zabibu katika mashamba ya Mpunguzi,Handali na Hombolo limeshuhudiwa na Naibu Waziri wa Kilimo Mh. Anthony Peter Mavunde

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments