SENEGAL YAFUZU KOMBE LA DUNIA, YAICHAPA MISRI KWA MIKWAJU YA PENATI


******************

NA EMMANUEL MBATILO

Senegal imefanikiwa kufuzu kombe la Dunia mara baada ya kufanikiwa kuwaondoa Misri kwa mikwaju ya penati baada ya kutoka kwa agg 1-1 kwenye mechi mbili nyumbani na ugenini.

Mechi ya kwanza ambayo ilipigwa nchiini Misri tulishuhudia Misri wakiondoka na ushindi wa bao 1-0 bao ambalo Senegal walijfinga kupitia kwa Saliou Ciss dakika ya 4 ya mchezo.

Katika raundi ya marudiano ambapo Senegal wakiwa nyumbani walipata bao kupitia kwa mshambuliaji wao Boulaya Dia dakika ya 3 ya mchezo na kuiwezesha timu yake kuibuka na ushindi kwenye mechi hiyo na matokeo yakawa agg 1-1.

Baada ya dakika 90 kumalizika ziliongezwa dakika 30 lakini milango yote haikuweza kufunguliwa mpaka hatua ya kupiga penati ikwadia.

Mohammed Salah miongoni mwa wachezaji waliokosa penati kwenye mechezo huo ambapo penati ya Sadio Mane iliwapeka moja kwa moja Senegal kushiriki michuano ya kombe la Dunia nchini Qatar.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments