MAKAMU WA RAIS WA IRAN ATHIBITISHWA KUAMBUKIZWA VIRUSI VYA CORONA


Makamu wa Rais wa Iran anayeshughulikia mambo ya wanawake na familia Bibi Masoumeh Ebtekar jana amethibitishwa kuambukizwa virusi vya Corona.

Mapema jana mwenyekiti wa kamati ya usalama wa taifa na sera za kidiplomasia wa Iran Bw. Mojtaba Zonnour, ambaye pia amethibitishwa kuambukizwa virusi, ametoa wito kwa raia wa Iran wawe watulivu na kusema, nchi yao ina uwezo wa kushinda mapambano dhidi ya virusi hivyo.

Habari zinasema, ibada ya sala ya ijumaa mjini Tehran imefutwa kutokana na mlipuko wa virusi hivyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527