JESHI LA POLISI KILIMANJARO LATAJA SABABU ZA KUMKAMATA MWENYEKITI WA CHADEMA FREEMAN MBOWE


Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro, Salum Hamdun amesema mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amekamatwa na polisi baada ya kutoa maneno ya uchochezi.

Amesema kiongozi huyo wa Kambi Rasmi ya Upinzani Bungeni ametoa maneno hayo leo Ijumaa Februari 28, 2020 katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika viwanja vya Nkoromu Masama kati wilayani Hai.

Amebainisha kuwa maneno aliyoyatoa mbunge huyo wa Hai yanaashiria  uchochezi  na kuamsha hisia za wananchi na chuki dhidi ya Serikali ya Tanzania na polisi.

"Mbowe amekamatwa na anashikiliwa na polisi baada ya kutuhumiwa kusema au kutoa maneno yanayoashiria uchochezi, kuamsha hisia na chuki dhidi ya Serikali na polisi. Anahojiwa lakini baada ya mahojiano atapewa haki ya dhamana,” amesema kamanda Hamdun.

Katika mkutano huo,  Mbowe amesema hawezi kupongeza utendaji kazi wa Serikali mpaka atakapokuwa na uhakika Serikali inatenda haki kwa watu wote.

Alikamatwa muda mfupi baada ya kumaliza mkutano wa hadhara saa 11:58 jioni.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527