BITEKO AKAGUA MIRADI YA MAENDELEO KWENYE JIMBO LAKE LA BUKOMBE



Mbunge wa Jimbo la Bukombe, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini akizungumza na wakazi wa Kata ya Uyovu jimboni humo Februari 28, 2020 kupitia mkutano wa hadhara uliofanyika katika Kijiji cha Buganzu.

Kabla ya mkutano huo, Biteko alikagua miradi mbalimbali ya maendeleo na kuwapongeza wananchi kwa kushirikiana kutekeleza miradi hiyo ikiwemo ujenzi wa vyumba vya madarasa na kuanzisha ujenzi wa Shule.
Baadhi ya wakazi wa Kata ya Uyovu jimboni Bukombe wakimsikiliza mbunge wao, Doto Biteko (hayuko pichani) ambaye pia ni Waziri wa Madini.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini alifika kukagua ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Lyobaika ambayo ujenzi wake umeanzishwa na wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini pia alikagua ujenzi wa Shule mpya ya Msingi Kapwani inayojengwa kwa nguvu za wananchi.
Mbunge wa Jimbo la Bukombe mkoani Geita, Doto Biteko ambaye pia ni Waziri wa Madini aliunga mkono juhudi za wananchi kwa kuahidi kuwasaidia ili kukamilisha miradi hiyo na mingine mingi jimboni Bukombe.
Tazama BMG TV hapa chini

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527