
Jaji Chande amebainisha hayo leo Alhamisi, Aprili 23, 2026, Ikulu Jijini Dar es Salaam, wakati wa hafla ya kukabidhi ripoti ya uchunguzi wa Tume hiyo kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, akitolea mfano wa picha iliyosambaa ikionesha mifuko yenye maiti zikidaiwa kuzikwa kwa halaiki.
Amesema: “Tume tuliweza kutofautisha picha halisi na zisizo halisi kwa kutumia utaalamu, kwa mfano mojawapo ni picha ambayo imetumika mara nyingi kuonesha maiti zikiwa kwenye mifuko ya buluu zikizikwa kwenye makaburi ya halaiki. Picha hiyo kwa mujibu wa uchunguzi imetumika sehemu nyingi duniani.”
Kwa mujibu wa Mwenyekiti huyo, Tume ilitumia ushahidi na taarifa mseto kutoka katika vyanzo mbalimbali ili kufikia viwango vya uthibitisho vinavyotambuliwa kimataifa, huku ikihakikisha uwepo wa ushahidi wa kujitosheleza.
Ameeleza kuwa katika uchunguzi huo wa kidijitali, Tume ilifanikiwa kukusanya jumla ya picha mnato 450 na picha mjongeo 880 kupitia njia mbalimbali, ikiwemo zile zilizosambaa mara nyingi mtandaoni, zilizowasilishwa na mashahidi, taarifa kutoka vyombo vya ulinzi na usalama, pamoja na vyanzo vya wazi kama vyombo vya habari na mitandao ya kijamii.
Social Plugin