Na mwandishi wetu,Dar es Salaam,
Leo Februari 27, 2026 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshiriki pamoja na viongozi mbalimbali katika Misa Takatifu ya kumuombea na kumuaga Askofu Mkuu Mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Dar es Salaam, Marehemu Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, iliyofanyika katika Kanisa Kuu la Mtakatifu Yosefu, Jijini Dar es Salaam.
Wananchi walioshiriki Misa hiyo wamesema kuwa mchango wa Kardinali Pengo utaendelea kuishi kupitia miradi ya kijamii, malezi ya vijana na uongozi wa kidini alioutoa kwa moyo mkunjufu.




Social Plugin