Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza rasmi matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne (CSEE) kwa mwaka 2025Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA) limetangaza matokeo ya Mtihani wa Taifa wa Kidato cha Nne 2025, uliofanyika kuanzia Novemba 17, 2025.
Matokeo hayo yametangazwa leo Januari 31, 2026, na Katibu Mtendaji wa NECTA, Profesa Said Mohammed, jijini Dar es Salaam.
Jumla ya watahiniwa 569,883 kutoka shule 5,864 pamoja na watahiniwa wa kujitegemea 25,927 walifanya mtihani huo, huku mahudhurio yakifikia asilimia 97.5.
NECTA imeeleza kuwa ufaulu umeongezeka kwa asilimia 2.61 na kufikia asilimia 94.98, ambapo watahiniwa 526,620 wamefaulu kwa kupata daraja la kwanza hadi la nne.
Aidha, watahiniwa 255,404 sawa na asilimia 46.1 wamepata daraja la kwanza hadi la tatu, hali inayoonesha kuimarika kwa ubora wa elimu ya sekondari nchini.

Social Plugin