Habari Mpya

6/recent/ticker-posts

MHANDISI JOHNSTON MTASINGWA AWAGARAGAZA 4 KURA ZA MAONI BUKOBA MJINI



Na Mariam Kagenda_Kagera 


Mhandisi wa TANROAD, Johnston Mtasingwa ameibuka mshindi katika Uchaguzi wa  Kura za maoni Jimbo la Bukoba Mjini  kwa kupata kura 1,408 na kuwabwaga wenzake  wanne waliokuwa wakishiriki mchakato wa kumpata Mbunge kupitia  Chama Cha Mapinduzi (CCM) 


Katibu wa Chama Cha Mapinduzi Jimbo la Bukoba Mjini, Shabani Mdohe ametangaza  matokeo ya kura za maoni ambapo amewataja wengine waliogombea kuwa ni Alex Denis ambaye amepata Kura  804 , Almasoud Kalumuna kura 640 Jamila Hassan kura 66 na Koku Rutha kura 44



 Wapiga kura waliojiandikisha ni 3033 waliojitokeza kupiga kura ni 2978 ambapo Kura  zilizoharibika ni kura 20 na kura halali ni 2958.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com