
Na Mwandishi wetu - Malunde 1 blog
Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Anamringi Macha, amewataka wanasiasa kuacha kutumia mfungo wa Ramadhani kujinufaisha kisiasa kwa kutumia kigezo cha kuandaa futari.
Aidha amewaomba waumini wa dini ya kiislamu na wakristo kutumia kipindi hiki cha mfungo kuombea taifa na watu wake hususani kuelekea kipindi uchaguzi mkuu ili kuwe na uchaguzi huru na haki ikiwa ni pamoja na kutumia sadaka zao kuwakumbuka waliopungukiwa na kuwafikia wahitaji.
Katika hatua nyingine amewataka wafanyabiashara kwenye masoko kuacha kujinufaisha kupitia kipindi hiki kwa kupandisha bei za mahitaji sokoni ili kuifanya funga kuwa nzuri ma yenye tija.
Social Plugin