BENKI YA CRDB YAKABIDHI MADAWATI URAMBO

Meneja wa Benki ya CRDB Kanda ya Magharibi,  Jumanne Wambura Wagana (kushoto) akimkabidhi madawati Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mh. Eribariki Bajuta.
Meneja wa CRDB Kanda ya Magharibi Ndg Jumanne Wambura Wagana amekabidhi madawati 50 kwa mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe.  Elibariki Bajuta ikiwa ni mwendelezo wa benki hiyo ya CRDB katika kutekeleza sera yake ya uwekezaji kwa jamii lakini kuunga mkono jitihada za Serikali kwenye sekta ya elimu wilayani Urambo. 

Akipokea Madawati hayo Aprili  4,2024, Mkuu wa Wilaya ya Urambo Mhe. Elibariki Bajuta ambaye aliambatana na Kamati ya Ulinzi na Usalama ya wilaya, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Urambo , Wakuu wa Idara wa Halmashauri pamoja na viongozi wengine ameishukuru sana Benki ya CRDB kwa msaada huo mkubwa na kuahidi kuendelea kuwapa mashirikiano makubwa zaidi kibiashara.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم