JKT TANZANIA , KAGERA SUGAR HAKUNA MBABE CCM KAMBARAGE

 



Na Mwandishi wetu _ Malunde 1 blog

Timu ya JKT Tanzania wametoka thuruhu ya goli 1 - 1 dhidi ya Kagera Sugar kwenye nmchezo wa ligi kuu NBC Tanzania Bara.

Mchezo huo uliochezwa leo Septemba 29, 2023 katika uwanjan wa CCM Kambarage Mjini Shinyanga uliomalizika kwa droo ya goli 1 - 1 huku magoli yote yakifungwa dakika za nyongeza  goli la JKT Tanzania likifungwa na Daniel Lyanga kwa mkwaju wa penati Dk 97 huki goli la Kagera Sugar likifungwa na Gasper Mwaipasi Dk 98.

Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa mchezo huo kocha msaidizi wa timu ya JKT Tanzania George Mketo amesema makosa waliyofanya baada ya kupata goli ndio limewaadhibu na kupelekea wapinzani wao kupata goli na kufanikiwa kusawazisha.

Kwa upande wake kocha msaidizi wa timu ya Kagera Sugar Marwa Chambeli amewapongeza wachezaji wake kwa kupambana na kufanikiwa kusawazisha goli na kugawana pointi kwenye mchezo huo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم