SIMBA SC YAKANDWA UARABUNI, YACHAPWA KWA MIKWAJU YA PENATI 4-3

NA EMMANUEL MBATILO,

KLABU ya Simba imetolewa na Wydad Casablanca kwenye mchezo wa mkondo wa pili wa hatua ya Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika (CAF CL). baada ya kupokea kichapo kwa mikwaju ya penati 4-3 mara baada ya matokeo kuwa 1-0 (agg 1-1)

Katika mchezo huo ambao Simba alikuwa na faida ya bao moja mbele, waliingia uwanjani na kikosi kilekile kilichoanza mkondo wa kwanza Jijini Dar es Salaam ambacho kiliwasaidia kuondoka na ushindi wa bao 1-0.

Mchezo huo uliopigwa katika dimba la Mohamed V nchini Morocco Wyadad waliweza kumuanzisha mshambuliaji wao hatari raia wa Senegal Bouly Sambou ambaye alionesha uhatari wake na kuweza kupata bao dakika ya 24 ya mchezo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
أحدث أقدم