KAMATI YA KUDUMU YA BUNGE YA MIUNDOMBINU YATEMBELEA NIT


Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Selemani Kakoso wakimsikiliza mmoja wa wakufunzi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya Kamati hiyo kufanya ziara kwenye Chuo hicho leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Selemani Kakoso wakimsikiliza mmoja wa wakufunzi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya Kamati hiyo kufanya ziara kwenye Chuo hicho leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Selemani Kakoso wakimsikiliza mmoja wa wakufunzi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya Kamati hiyo kufanya ziara kwenye Chuo hicho leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam. Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Selemani Kakoso wakimsikiliza mmoja wa wakufunzi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya Kamati hiyo kufanya ziara kwenye Chuo hicho leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam.Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu Mhe. Selemani Kakoso akizungumza wakati Kamati hiyo ilipotembelea Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam.Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya akizungumza mara baada ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kutembelea Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) leo Machi 17, 2023 Jijini Dar es SalaamMkuu wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT) Prof. Zakaria Mganilwa akizungumza wakati Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake, Mhe. Selemani Kakoso walipotembelea Chuo hicho leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam. Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakiwa katika Kikao na Watumishi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya kamati hiyo kufanya ziara Chuoni hapo leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam. Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakiwa katika Kikao na Watumishi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya kamati hiyo kufanya ziara Chuoni hapo leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam.

Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakiwa katika Kikao na Watumishi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya kamati hiyo kufanya ziara Chuoni hapo leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam. Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu wakiwa katika Kikao na Watumishi wa Chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) mara baada ya kamati hiyo kufanya ziara Chuoni hapo leo Machi 17,2023 Jijini Dar es Salaam.

(PICHA ZOTE NA EMMANUEL MBATILO)

***************************************

-Yavitaka Vyuo Vingine vilivyo chini ya Wizara kuongeza nguvu

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeishauri Serikali kuongeza Uwekezaji katika vyuo vinavyozalisha wataalamu kwenye sekta ya Ujenzi na Uchukuzi ili kutoa wahitimu wenye sifa zinazohitaji kwenye soko la ajira kwa manufaa ya Taifa hapo baadae.

Ushauri wa Kamati hiyo umetolewa na Mwenyekiti wake Mhe. Selemani Kakoso mara baada ya kufanya ziara ya kuvitembelea Vyuo vya kisekta na kupokea taarifa ya utekelezaji wa Maendeleo ya Chuo Cha Bandari, Chuo cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT), Chuo Cha Hali ya Hewa,Chuo Cha Reli,Chuo Cha Usafiri wa Anga na Chuo Cha Bahari (DMI).

Ameeleza kulidhishwa na Maendeleo na Mikakati ya Chuo Cha Taifa Cha usafirishaji NIT huku akivitaka vyuo vingine vilivyo chini ya Wizara ya Ujenzi na uchukuzi kuongezewa nguvu ili viweze kutoa mafunzi kulingana na mahitaji ya Sasa.

Nae Mkuu wa chuo Cha Taifa Cha Usafirishaji (NIT) Prof. Zacharia Mganilwa ameishukuri Kamati ya Bunge ya Miundombinu na kusema kuwa maelekezo waliyopewa na Kamati hiyo watayasimamia kikamilifu ili kufikia matarajio yanayokusudiwa.

Naibu waziri wa Ujenzi na uchukuzi Mhandisi Godfrey Kasekenya amevitaka vyuo hivyo kutokuwa na uoga pindi Kamati za bunge zinapopita kukagua maendeleo ya vyuo vyao badala yake wawe huru na waeleze matatizo yao ili wasaidiwe huku Mkuu wa chuo Cha Usafiri wa Anga akisema maelekezo yaliyotolewa na Kamati hiyo Kwa Chuo chake ni mazuri na watayasimamia vyema kwasababu yanalenga Kuboresha zaidi

Pamoja na mambo mengine Kamati ya kudumu ya Bunge ya Miundombinu imeipongeza serikali Kwa hatua mbalimbali za kuimarisha sekta ya ujenzi na uchukuzi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments