DITOPILE AMLIPUA LEMA, AMTAKA AJITOKEZE KUOMBA RADHI


Mbunge wa Viti Maalumu Mkoa wa Dodoma Mhe. Mariam Ditopile amemtaka aliyekuwa Mbunge wa Jimbo la Arusha Mjini kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Godbless Lema ajitokeze aombe radhi kutokana na kauli yake aliyoitoa kuhusu Vicoba ambayo ni ya kuwadhihaki wanawake.

Katiba hotuba yake Lema alikaririwa  akisema Vicoba ni umasiki na ndio maana alimwondoa mkewe kwenye benki hizo.


Ditopile ametoa wito huo alipo kuwa mgeni rasmi katika kongamano la Vicoba na kumpongeza Rais Dk. Samia Suluhu Hassan kwa  kutimiza miaka miwili madarakani  liloandaliwa na Shirika la Msaada wa Kisheria (JUST).

“Kama kweli tunataka kurekebisha pale ambapo serikali imekosea basi tuwe na lugha nzuri,kama kuna mtu anaona vikoba havifai basi aje na hoja zake  sio kudharau kwasababu wapo wanawake wengi wanaendesha shughuli zao kupitia fedha hizo kidogo",alisema.


Amesema “Ndugu yangu huyu Godbless Lema kiukweli ametumia lugha ambayo   imetudhihaki sisi wanawake na inawezekana hata mama yake alikuwa ni miongoni na kama anahoja aishauri serikali"


"Mimi namuomba ashuke chini akafuatilie vikoba hivi ni kwa namna gani vimeinua maisha ya watanzania ajifunze na kama anaona kuna sehemu ya kujirekebisha aseme, ikiwezekana atoke na afute kauli yake kwasababu ametukosea sana, asitumie uhuru vibaya aliopewa na Rais Dkt. Samia",ameongeza.


Ditopile amesisitiza kuwa uanzishwaji wa huduma ndogo za fedha  upo kwa mujibu wa sheria ambayo ilitungwa wakati Godbless Lema akiwa Mbunge. 

Alisema wizara ya fedha ilitunga sheria ya huduma ndogo za fedha mwaka 2017 lengo ni kuhakikisha huduma hiyo inaleta tija kwa wananchi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments