JESHI LA POLISI LAMSHUKURU RAIS  SAMIAKUBORESHA MAZINGIRA YA UTOAJI MAFUNZO YA KITAALUMA


********************

Na mwandishi wetu Jeshi la Jeshi la Polisi

Jeshi la Polisi Nchini linamshukuru mheshimiwa Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Daktari Samia Suluhu Hassan kwa kuboresha utaratibu katika mafunzo ya Jeshi hilo kwa kuwawezesha vitendea kazi ikiwa nipamoja na kuondoa makato ya fedha ya chakula kwa askari walioko mafunzoni katika vyuo mbalimbali vya Jeshi hilo.

Hayo ya mesemwa leo march 01 2023 na Kamishina wa opereshi na mafunzo ya Jeshi la Polisi Nchini CP AWADHI JUMA HAJI alipokuwa akiongea na wanafunzi wa kozi ya uofisa na mkaguzi msaidizi wa Polisi katika chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam ambapo amebainisha kuwa hapo awali kulikuwa na utaratibu wa askari kukatwa fedha anapokuwa mafunzoni.

Aidha Kamishina Awadhi amewataka askari hao kujitoa kikamilifu katika mafunzo hayo kwa kupokea mafunzo yanayotolewa na walimu ndani ya darasa na katika medani za kivita ili kutimiza adhima ya amiri Jeshi ya kujenga mazingira rafiki katika kozi za Jeshi hilo.

Sambamba na hilo ujio wake pia ni katika kuungana na kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi Jamal Rwambow ambae ni mstaafu wa Jeshi la Polisi ambapo amebainisha kuwa kamishina uyo amejikita katika uandishi wa vitabu lengo likiwa ni kuikomboa jamii kupitia uandishi wake na kushauri Jeshi la Polisi katika utoaji huduma kwa wananchi.

Pia katika hafla hiyo amepata wasaa wa kuzindua kitabu kilichoandikwa Salam za marehemu nakuwaomba askari kusoma vitabu hivyo ambavyo vina toa dira na mweleko sahihi katika kutoa huduma kwa jamii.

Kwa upande wake kamishina msadizi mwandamizi mstaafu Jamal Rwambow amesema kuna baadhi ya watu wanasimamia kazi za upelelezi ambapo amebainisha kuwa kuna watu hao hawana uwezo mkubwa wa maswala ya upelelezi na kusema kuwa Jeshi hilo linaouwezo mkubwa wa upelelezi hivyo ameiomba serikali kuliwezesha kifedha hasa kitengo cha upelelezi ili kuwa naufanisi mkubwa.

Nae mkuu wa chuo cha Taaluma ya Polisi Dar es salaam Kamishina msaidizi mwandamizi wa Polisi Daktari LAZARO MAMBOSASA amesema kuwa anamshukuru mkuu wa Jeshi la Polisi kwa namna anavyopigania maslahi ya askari na kuahidi kuwa wao kama wakufunzi watahakikisha wanasimamia mafunzo hao kwa weledi mkubwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments