TWIGA MINERALS NA BARRICK WADHAMINI MKUTANO WA JUKWAA LA PILI LA UTEKELEZAJI WA USHIRIKISHWAJI WATANZANIA KATIKA SEKTA YA MADINI


Meneja wa Barrick nchini, Dk. Melkiory Ngido (katikati) akifuatilia mada za ufunguzi wa mkutano huo,(kushoto) kwake ni Afisa Mwendeshaji Mkuu wa kampuni ya Max Steel,Purvita Vadgama na (kulia) ni Mhasibu Mwandamizi wa kampuni ya Apex,Christina Padilla. Barrick na Twiga ni wadhamini wakuu wa mkutano huo
Baadhi ya washiriki wa mkutano huo wakifuatilia matukio
Watendaji Waandamizi kutoka taasisi mbalimbali wakibadilishana mawazo nje ya ukumbi wa mkutano huo.
Watendaji Waandamizi kutoka taasisi mbalimbali wakibadilishana mawazo nje ya ukumbi wa mkutano huo.
Wajumbe wa mkutano wakifuatilia mawasilisho ya mada mbalimbali za ufunguzi.


Kampuni ya Serikali Twiga Minerals Corporation, yenye ubia na kampuni ya kampuni ya uchimbaji wa madini ya dhahabu ya Barrick Gold Corporation, ni mdhamini mkuu wa mkutano wa Jukwaa la Pili la utekelezaji wa ushirikishwaji Watanzania katika sekta ya madini.


Mkutano huu unaofanyika kila mwaka umeandaliwa na Serikali kupitia Tume ya Madini chini ya Wizara ya Madini na unafanyika katika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Arusha International Conference Centre (AICC), na kukutanisha wadau mbalimbali kutoka sekta hiyo ya madini kwa lengo la kujadili na kufanya tathmini ya ushirikishwaji watanzania katika mnyororo wa sekta hiyo.

Waziri wa Madini, Mh. Dkt. Doto Biteko, anatarajia kuwa mgeni rasmi katika uzinduzi wa mkutano huo kesho.


Mkutano huo wenye kauli mbiu ya “Ushirikishwaji wa Watanzania katika sekta ya madini kwa kufungamana na sekta nyingine kwa uchumi imara wa nchi” unaambatana na maonyesho ya makampuni mbalimbali yanayojihusisha na shughuli za uchimbaji wa madini nchini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments