ACHOMWA MKUKI AKIFUKUZA MIFUGO SHAMBANI



Mohamed Salumu (44) mkazi wa Kijiji cha Olpopong kata ya Njoro wilayani Kiteto mkoani Manyara amenusurika kifo kwa kuchomwa mkuki kifuani wakati akizuia mifugo isiharibu mazao yake shambani.


Watuhumiwa hao waliamuru mifugo hiyo iharibu mazao hayo shambani ambapo jumla ya ekari 6 zimeteketezwa na mifugo hiyo.

Awali vijana hao walifika kwa mkulima huyo na kufungua uzio uliokuwa umewekwa hapo shambani na baada ya kuzuiwa mkulima huyo walimrushia mkuki ambao umemjeruhi kifuani na kwa sasa majeruhi huyo amelazwa hospitali ya wilaya ya Kiteto kwa matibabu zaidi.

Via EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments