BARRICK YAKABIDHI GARI LA WAGONJWA 'AMBULANCE' KITUO CHA AFYA BUGARAMA


Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (kulia) wakikata utepe wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Kampuni ya Uchimbaji Madini ya Dhahabu ya Barrick imechangia gari maalumu la kubebea wagonjwa 'Ambulance' katika Kituo cha afya Bugarama kilichopo kata ya Bugarama Halmashauri ya wilaya ya Msalala Mkoani Shinyanga.


Gari hilo limekabidhiwa leo Jumatano Machi 22,2023 na
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow kwa Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita.


Akizungumza wakati wa hafla fupi ya makabidhiano ya gari hilo iliyofanyika katika Kituo cha Afya Bugarama, Bristow amesema Barrick inathamini suala la usalama na afya katika jamii ndiyo maana imeamua kutoa gari hilo kama sehemu ya mchango wao katika kuboresha huduma za afya kwa jamii inayozunguka mgodi wa Barrick Bulyanhulu uliopo katika Halmashauri ya Msalala.


"Gari hili tumelitoa kama sehemu ya mchango wetu kwa jamii ni nje ya Fedha za mfuko wa uwajibikaji kwa jamii,tunaamini litasaidia katika kuboresha huduma za afya kwa wananchi. Tutahakikisha tunaendelea kushirikiana na  jamii inayozunguka migodi yetu", amesema Bristow.

Kwa upande wake, Mkuu wa wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita ameishukuru Kampuni ya Barrick kwa namna inavyojitahidi kutekeleza miradi  mingi inayogusa wananchi huku akisisitiza kuwa serikali itaendelea kushirikiana na Wawekezaji ili kuwaletea maendeleo wananchi.


"Tunawashukuru Barrick kwa kutekeleza ahadi ya kuleta Ambulance katika kituo hiki cha Afya Bugarama. Gari hili litasaidia kutatua changamoto zilizopo...Nasi tunaahidi kutunza na kutumia gari hili kwa malengo yaliyokusudiwa. Ambulance hii itaongeza nguvu katika utoaji wa huduma za afya", amesema Mhita.

"Barrick wamekuwa wadau wakubwa katika wilaya ya Kahama, wana miradi mingi inayogusa wananchi na hii inatokana na ushirikiano mzuri uliopo baina ya Serikali na Kampuni ya Barrick", ameongeza.


Nao Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Leonard Mabula na Diwani wa Kata ya Bugarama, Mhe. Prisca Msoma wameishukuru Barrick kwa kutekeleza kwa wakati ombi la Ambulance ili kutatua changamoto ya huduma za matibabu katika kituo hicho cha afya kinachohudumia jamii ya Bugarama na maeneo ya jirani ikiwemo Geita.


Mganga Mfawidhi wa Kituo cha afya Bugarama Dkt. Silas Kayanda na Mganga mkuu wa Halmashauri ya Msalala Dkt. Sisti Mosha wamesema walitoa ombi la kupatiwa Ambulance kutoka Barrick mnamo Januari 25,2023 huku wakieleza kuwa kupatikana kwa gari hilo kutapunguza changamoto ya usafiri kwa wagonjwa katika kituo hicho cha afya.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (kulia) wakikata utepe wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (kulia) wakikata utepe wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow akimkabidhi Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita funguo ya gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (kulia) wakishikana mkono wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (kulia) wakishikana mkono wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Muonekano wa gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Muonekano wa gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Meneja Mkuu wa Mgodi wa Barrick Bulyanhulu, Cheick Sangare akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Kaimu Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Msalala Leonard Mabula akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Diwani wa Kata ya Bugarama Mhe. Prisca Msoma akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mganga mkuu wa Halmashauri ya Msalala Dkt. Sisti Mosha akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Mganga Mfawidhi wa Kituo cha afya Bugarama Dkt. Silas Kayanda akizungumza wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.

Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow akizungumza jambo na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita wakati wa hafla fupi ya kukabidhi gari la kubebea wagonjwa katika kituo cha afya Bugarama kilichopo katika Halmashauri ya Msalala.
Wadau wakifuatilia matukio yaliyokuwa yanaendelea
Awali Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow akisalimiana na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita (kushoto).
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita wakipiga picha na viongozi mbalimbali wa Kampuni ya Barrick na Serikali
Mtendaji Mkuu ambaye pia ni Rais wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation Mark Bristow na Mkuu wa Wilaya ya Kahama Mhe. Mboni Mhita wakipiga picha na wadau mbalimbali.


Picha zote na Kadama Malunde - Malunde 1 blog


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments