MFALME ZUMARIDI AFUNGUKA ALIVYOUGUA PRESHA GEREZANI




Mhubiri, Diana Bundala maarufu "Mfalme Zumaridi" amefunguka magumu aliyopitia akiwa gerezani kuwa ni pamoja na kuugua ugonjwa wa shinikizo la damu 'presha' ambao hakuwa nao, huku akitengwa na baadhi ya wafungwa wenzake.


Zumaridi ametoa kauli hiyo leo nyumbani kwake baada ya kumaliza kifungo chake cha mwaka mmoja katika Gereza la Butimba jijini Mwanza baada ya Mahakama ya Hakimu Mkazi Mkoa wa Mwanza kumtia hatiani katika shtaka la kuzuia maofisa wa serikali kutekeleza majukumu yao.




Amesema hatasahau miezi 10 ya mwanzo kati ya 11 aliyokaa ndani ya gereza hilo tangu alipokamatwa kutokana na baadhi ya wafungwa kumtenga jambo lililomnyima amani ndani ya gereza hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments