CPB YAJIPANGA KUPAMBANA NA UPANDAJI WA BEI ZA MAZAO


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

BODI ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko (CPB),imesema imejipanga kuhakikisha wanapambana katika kupunguza upandaji wa mazao mbalimbali kwa kuwasaidia wakulima upatikanaji wa mbolea kwa wakati,

Hayo yamebainishwa leo Februari 11,2023 Jijini Dar es Salaam na Mwenyekiti wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko(CPB), Salum Hagan,wakati wa mkutano wa wadau wa bodi hiyo ulifanyika Ubungo jijini hapa .

Hagan amesema kupanda kwa chakula kinatokana na changamoto mbalimbali ikiwe upatikanaji hafifu kwa mbolea kunakochangiwa na hali ya Vita ya Ukrani na Urusi hivyo baada ya kuliona ilo Bodi hiyo na kusaidia upatikani wa mbolea kilahisi kwa wakulima na kupelekea kufanya kilimo kwa wingi na kusaidia kupungua kwa upandaji wa vyakula.

Mbali na jitihada hizo,Hagan amesema kwa sasa bodi inapanga kununua mazao kwa wingi kutoka kwa wakulima na kuweka ziada ya chakula ambapo amesema bodi hiyo inaweza kununua mazao yenye thamani ya bilioni 50 huku ikitarajia kuongeza kiasi hicho cha fedha na kufikia bilioni 100.

Hata hivyo,Hagan,amesema baada kuteuliwa kuongoza bodi hiyo kwa kipindi kifupi wameweza kubadili mifumo mbalimbali ndani ya bodi pamoja na kuwaita wadau kufanya kazi na CPB.

Kwa Upande wake Mstahiki Meya wa Ubungo na Diwani wa Kata ya Ubungo. Mh.Mwasha Hassan Siraju,ambaye alikuwepo kwenye mkutano huo na amempongeza mwenyekiti wa bodi ya CBP kuteuliwa kwenye nafasi na kusema bodi itakwenda kutatua changamoto ya upandaji wa mazao unaendelea hapa nchini.

Mwenyekiti wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko(CPB), Salum Hagan akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa bodi hiyo ulifanyika leo Februari 11,2023 Ubungo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko(CPB), Salum Hagan akisisitiza jambo wakati akizungumza katika mkutano wa wadau wa bodi hiyo ulifanyika leo Februari 11,2023 Ubungo jijini Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko(CPB), Salum Hagan akizungumza wakati wa mkutano wa wadau wa bodi hiyo ulifanyika leo Februari 11,2023 Ubungo jijini Dar es Salaam.

Wadau wa Bodi ya Nafaka na Mazao Mchanganyiko(CPB) wakifuatilia mkutano ambao umefanyika leo Februari 11,2023 Jijini Dar es Salaam

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments