TANZANIA GIRL GUIDES ASSOCIATION WAENDESHA KAMPENI YA UPANDAJI MITI SHULE YA MSINGI NDEMBEZI

 

Wakala Mtetezi wa Mradi wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka Tanzania Girl Guides Association

Kampeni ya upandaji miti ikiendelea katika shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.


Na Marco Maduhu, SHINYANGA

CHAMA kisicho cha kiserikali Tanzania Girl Guides Association kimeendesha Kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga, ili kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na athari za mazingira.

Kampeni hiyo imefanyika leo Februari 3, 2023 ikiwa ni mwendelezo wa Kampeni ya kuhamasisha wananchi kupanda miti kwenye Kaya zao, pamoja na Taasisi za Serikali zikiwamo shule za Msingi na Sekondari, huku Mgeni Rasmi akiwa ni Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji mkoani Shinyanga Beda Chamatata, akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa huo.

Akizungumza kwenye Kampeni hiyo ya upandaji Miti Wakala Mtetezi wa Mradi wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka Tanzania Girl Guides Association, Joyce Maganga, amesema kampeni hiyo ya upandaji miti ilianza Rasmi mwaka 2021, na wameshapanda miti mingi katika shule za Msingi Manispaa ya Shinyanga.

Amesema upandaji miti katika shule hiyo ya Msingi Ndembezi ni mwendelezo wa Kampeni ambayo wamekuwa wakiiendesha mashuleni kupanda miti, ambapo wameshapanda pia miti 300 katika shule ya Msingi Ujamaa, Miti 200 shule ya Msingi Jomu.

“Leo katika Shule hii ya Msingi Ndembezi tumepanda Miti zaidi ya 1,000, na kampeni hii ni endelevu ili kuunga mkono juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan ya kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi na athari za mazingira,”amesema Maganga.

“Nawaomba viongozi na watoa maamuzi katika vikao vyenu ajenda ya kuhamasisha wananchi kupanda miti hasa katika msimu wa mvua iwe ya kudumu, ili ipandwe miti mingi ya kutosha na kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi,”ameongeza.

Naye Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura, amepongeza kampeni hiyo ya upandaji miti ambayo itasaidia kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi pamoja na kupata mvua za kutosha na kuondokana na hali ya ukame.

Mgeni Rasmi Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji mkoani Shinyanga Beda Chamatata, akimwakilisha Katibu Tawala wa Mkoa huo, amewataka wanafunzi kuitunza miti hiyo ili ikue na kuwapatia faida mbalimbali ikiwamo kivuli na kuzuia mmomonyoko wa udongo.

Ametaja faida nyingine ya miti ni kuondoa hewa ya ukaa na kupata hewa nzuri, huku akiwaagiza viongozi kuwachukulia hatua kali wafugaji ambao wamekuwa wakipitisha mifugo kwenye maeneo yaliyopandwa miti.

Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji mkoani Shinyanga Beda Chamatata, akizungumza kwenye kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Ndembezi.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura, akizungumza kwenye kampeni ya upandaji miti katika shule ya msingi Ndembezi.

Wakala Mtetezi wa Mradi wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka Tanzania Girl Guides Association, Joyce Maganga, akizungumzia namna wanavyoendesha kampeni ya upandaji miti.

Mwalimu Mkuu wa shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga Mohamed Makana, akizungumza kwenye Kampeni ya upandaji Miti

Kamishina wa Skauti Bi. Suzani Kidima akizungumza kwenye Kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.

Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Ndembezi Rubeni Dotto akizungumza kwenye Kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.

Afisa Maliasili na Mazingira Manispaa ya Shinyanga Ezra Manjerenga akizungumza kwenye kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga.

Mwanafunzi Noelina Busisi akitoa elimu ya umuhimu wa upandajimiti kwa wananafunzi wenzake ili wawe Mabalozi wazuri wa kupinga uharibifu wa mazingira.

Wakala Mtetezi wa Mradi wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka Tanzania Girl Guides Association, Joyce Maganga, akizungumzia namna wanavyoendesha kampeni ya upandaji miti.

Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji mkoani Shinyanga Beda Chamatata, akizungumza kwenye kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Ndembezi.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura akipanda mti katika shule ya Msingi Ndembezi.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga wakipanda mti.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Zoezi la upandaji miti likiendelea.

Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji mkoani Shinyanga Beda Chamatata, akizungumza kwenye kampeni ya upandaji miti katika shule ya Msingi Ndembezi, akiwa na Wakala wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia Nchi Joyce Maganga, wakipiga picha na wanafunzi.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye Kampeni ya upandaji miti.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye Kampeni ya upandaji miti.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye Kampeni ya upandaji miti.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga wakiwa kwenye Kampeni ya upandaji miti.

Wanafunzi wa shule ya Msingi Ndembezi Manispaa ya Shinyanga wakitoa burudani kwenye Kampeni ya upandaji miti.

Walimu wakiwa kwenye Kampeni ya upandaji miti.

Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kampeni ya Upandaji Miti.

Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kampeni ya Upandaji Miti.

Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kampeni ya Upandaji Miti.

Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye Kampeni ya Upandaji Miti.

Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji mkoani Shinyanga Beda Chamatata, (kushoto) akipiga picha ya pamoja na Wakala Mtetezi wa Mradi wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka Tanzania Girl Guides Association Joyce Maganga.

Katibu Tawala msaidizi sehemu ya uchumi na uzalishaji mkoani Shinyanga Beda Chamatata, (kushoto) akipiga picha ya pamoja na Wakala Mtetezi wa Mradi wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka Tanzania Girl Guides Association, Joyce Maganga.

Mkurugenzi wa Manispaa ya Shinyanga Jomaary Satura (kushoto) akipiga picha ya pamoja na Wakala Mtetezi wa Mradi wa Msichana na Mabadiliko ya Tabia nchi kutoka Tanzania Girl Guides Association, Joyce Maganga.

Picha na pamoja zikiendelea kupigwa.

Picha na pamoja zikiendelea kupigwa.

Picha na pamoja zikiendelea kupigwa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments