AVAMIA KANISA KATOLIKI GEITA, AHARIBU VITU VITAKATIFU


Sehemu ya uharibifu uliofanywa

NA ROSE MWEKO, GEITA
MTU asiyefahamika amevamia na kuingia ndani ya kanisa Katoliki jimbo la Geita na kufanya uharibifu katika altare na sakrestia na kuvunja tabernakulo, kumwaga ekaristi takatifu na kuchana kitabu kitakatifu Biblia sambamba na kuharibu mfumo wa camera za ulinzi.

Taarifa iliyotolewa na Askofu wa Jimbo Katoliki la Geita kwa njia ya simu Flavian Matindi Kasalla amesema mtu huyo alivunja kioo cha mlangoni na kuharibu madhabahu takatifu huku akiharibu sehemu mbalimbali za ibada na kuharibu vitabu vitakatifu.
“Mpaka sasa hatujajua alikotokea na wala hatujui aliingia saa ngapi japo ilikuwa ni usiku wa kuamkia siku ya Jumapili, kanisa letu linalindwa na kampuni ya ulinzi ila mpaka sasa ni kitendawili kuwa mlinzi alikuwa wapi.

Mtu aliyefanya tukio hilo amekamatwa na ameshafikishwa katika vyombo vya usalama pamoja na mlinzi aliyekuwa zamu siku hiyo” amesema Askofu Kasalla.
Watu wawili wanashilikiwa na jeshi la Polisi kwa mahojiano zaidi.

 Akithibithisha kukamatwa kwa watu hao, Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita ACP Berthaneema Mlay amesema jeshi la Polisi linaendelea na uchunguzi zaidi ili kubaini nani kamtuma na sababu za kufanya uharibifu huo.
“Mtu huyo anaonekana alikuwa mlinzi na ni mtu ambaye amekuwa akihudumu katika kanisani haswa huko alikotoka Bukoba hivyo jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi na itakapobainika tutatoa taarifa zaidi kwani mpaka sasa kuna mambo tunayafuatilia tatutayazungumza ili kutovuruga upelelezi.

Chanzo - The Profiletv blog

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments