BIBI AWACHOMA MOTO WATOTO WA MWANAMKE ALIYEMUOA


Mmoja kati ya watoto watatu waliochomwa moto


Watoto watatu wa familia moja wilayani Rorya mkoani Mara, wamelazwa katika hospitali ya wilaya ya Shirati wakipatiwa matibabu kwenye majeraha mbalimbali ya moto waliyochomwa na mwanamke anayedaiwa kuwa ni bibi yao aitwaye Eliza Odira (68).


Taarifa zimeeleza kuwa bibi huyo amemuoa kimila mama wa watoto hao (Nyumba ntobhu)ili amzalie watoto na kwamba chanzo cha ukatili huo bado hakijajulikana na bibi huyo yupo kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi.

Akizungumza baada ya kutembelea watoto hao, Mkuu wa Wilaya ya Rorya, Juma Chikoka, amesema kuwa bibi huyo anadaiwa kuwafanyia watoto hao vitendo vya kikatili kwa muda mrefu na kwamba baada ya taarifa hizo kupatikana polisi walifika nyumbani kwake na kuwakuta watoto hao wakiwa katika hali mbaya na kulazimika kuwawahisha hospitalini huku bibi huyo akipelekwa kituo cha polisi kwa mahojiano.

Via EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments