RAIS SAMIA AFANYA MABADILIKO BARAZA LA MAWAZIRI, MAKATIBU WAKUU
الثلاثاء, فبراير 14, 2023
Rais Samia Suluhu Hassan amefanya mabadiliko madogo katika Baraza la Mawaziri, ambapo amemhamisha Mohamed Mchengerwa aliyekuwa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo kwenda kuwa Waziri wa Maliasili na Utalii.
Kupitia taarifa iliyotolewa leo Jumanne Februari 14, 2023 na Mkurugenzi wa mawasiliano ya Rais ikulu Zuhura Yunus imeeleza kuwa Kabla ya mabadiliko hayo nafasi hiyo ya Waziri wa Maliasili na Utalii illikuwa ikishikiliwa na Dkt. Pindi Chana.Dkt. Pindi Chana amehamishiwa Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Pia Dkt. Samia amefanya mabadiliko madogo kwa Makatibu Wakuu wa wizara ambapo Dkt. Hassan Abbasi amehamishwa na kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Maliasili na Utalii akitokea wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Nafasi hiyo ilikuwa ikishikiliwa na Profesa Eliamani Sedoyeka.
Said Othman Yakub ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu wa wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo nafasi iliyokuwa ikishikiliwa na Dkt. Abbasi.
Kabla ya uteuzi huo Yakub alikuwa Naibu Katibu Mkuu wa wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Viongozi hao wataapishwa hapo kesho saa 10 jioni Ikulu, Dar es Salaam.
Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundeblog@gmail.com
🚧🚦 Usiendeshe gari lako bila Mafunzo na Leseni halali_ 📲 Wasiliana nasi sasa: wa.me/255740273285 Unahitaji nini? 🚘 Unataka kujifunza udereva wa magari na kupata Cheti? 📄 Una cheti unataka kupata Leseni? 🔄 Unajua kuendesha lakini huna cheti wala leseni na unataka refresh upate cheti? 🛣️ Una nyaraka zote muhimu lakini unahitaji kujifua zaidi barabarani? ✅ Una Leseni bila cheti na unataka renew? 🌍 Tupo mikoa yote Tanzania hadi vijijini! 📞 Tupigie sasa: 0769 763 285
Social Plugin