ORODHA YA WAPISHI WA CAKE SHINYANGA 'SHY BAKERS', NAMBA ZA SIMU HIZI HAPA



Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog

Kikundi cha Wapishi wa Keki (Cake Bakers) Manispaa ya Shinyanga kimefanya Sherehe Maalum ‘Shy Bakers White Party 2023’ kufungua rasmi Mwaka 2023 na kupanga mikakati mbalimbali ya kutanua wigo wa kazi yao.

Sherehe hiyo iliyofanyika Jumatatu Februari 6,2023 katika ukumbi wa Green View uliopo Kambarage Mjini Shinyanga imehudhuriwa na wanachama wa kikundi hicho cha Wapishi maarufu wa Keki na wapambaji wa keki katika Manispaa ya Shinyanga.

Akizungumza wakati wa sherehe hiyo, Mwenyekiti wa Kikundi cha Wapishi wa Keki katika Manispaa ya Shinyanga Bi. Tabitha Mdongo maarufu ‘Binti Mdongo Cake’ amesema wameamua kufanya sherehe ili kufungua rasmi mwaka 2023.

“Sisi wapambaji wa keki na wapishi wa keki za aina na shughuli mbalimbali tumekutana kwa ajili ya kufungua rasmi mwaka 2023 kwa kujadili maendeleo ya kikundi chetu lakini pia kupanga mikakati mbalimbali jinsi ya kutanua wigo wa kazi yetu. Tumekula chakula cha pamoja, tumekunywa, tumecheza muziki, kubadilishana mawazo na kupeana zawadi”,ameeleza Tabitha.

Tabitha ametumia fursa hiyo kuwaomba wateja kuendelea kupata huduma ya keki zinazotengenezwa na wanachama wa kikundi hicho huku akiwakaribisha wapishi wengine wa keki kujiunga na kikundi chao.

Mwenyekiti wa Kikundi cha Wapishi wa Keki katika Manispaa ya Shinyanga Bi. Tabitha Mdongo akizungumza wakati wa Shy Bakers White Party 2023 iliyofanyika Jumatatu Februari 6,2023 Mjini Shinyanga. Picha na Kadama Malunde  - Malunde 1 blog
Mwenyekiti wa Kikundi cha Wapishi wa Keki katika Manispaa ya Shinyanga Bi. Tabitha Mdongo akizungumza wakati wa Shy Bakers White Party 2023 iliyofanyika Jumatatu Februari 6,2023 Mjini Shinyanga.
Wanachama wa Kikundi cha Wapishi wa Keki katika Manispaa ya Shinyanga wakionesha Keki Maalumu waliyoiandaa kwenye Shy Bakers White Party 2023.
Wanachama wa Kikundi cha Wapishi wa Keki katika Manispaa ya Shinyanga wakionesha Keki Maalumu waliyoiandaa kwenye Shy Bakers White Party 2023.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments