MAMA ADAIWA KUMUUA MTOTO WAKE KWA KIPIGO


Jeshi la Polisi mkoa wa Mbeya, linamshikilia Joyce Matingo (26), mkazi wa Unyamwanga wilaya ya Rungwe, mkoani Mbeya kwa tuhuma za kumuua mtoto wake aitwaye Emily Matingo(9) kwa kumpiga sehemu mbalimbali za mwili wake.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, Kamishna Msaidizi wa Jeshi la Polisi ACP Benjamin Kuzaga, amesema kuwa tukio hilo limetokea Januari 8 mwaka huu majira ya saa 12:00 jioni.

Kamanda Kuzaga ametoa wito kwa wazazi na walezi kuacha tabia ya kujichukulia sheria mkononi ikiwa ni pamoja na kutoa adhabu zilizopitiliza na kusababisha madhara makubwa ikiwemo na kutoa uhai wa wengine.


Via: EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments