UVCCM SHINYANGA WAADHIMISHA MIAKA 46 YA CCM

Madhimisho ya miaka 46 ya Chama Cha Mapinduzi CCM

Na Marco Maduhu, SHINYANGA

UMOJA wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (UVCCM) mkoa wa Shinyanga, umeadhimisha miaka 46 ya kuzaliwa kwa Chama Cha Mapinduzi (CCM), huku vijana wa chama hicho wakitakiwa kuanzisha miradi ya maendeleo ili wajikwamue kiuchumi.

Madhimisho hayo yamefanyika leo Januari 25 katika ukumbi wa Mikutano wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wilaya ya Shinyanga Mjini, na katika maadhimisho hayo kulikuwa na matukio ya kupanda miti katika Shule mpya ya Sekondari Lubaga, na kutoa misaada mbalimbali katika kituo cha kulea watoto wenye ulemavu Buhangija.

Akizungumza katika maadhimisho hayo mgeni rasmi Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana Ramadhani Mlao, amewataka vijana wa chama hicho (UVCCM) waanzishe miradi ambayo itawainua kiuchumi.

“Vijana lazima tujishughulishe vinginevyo tutaendelea kuwa vibara wa watu, hakuna kitu kibaya kama kuwa omba omba kutakufanya uwe mnyonge, tumieni fursa zilizopo ikiwamo kuanzisha miradi ya kilimo,”amesema Mlao.

Katika hatua nyingine amewataka vijana wa Chama hicho, wawe mstari wa mbele kukipigania chama kupitia mikutano ya hadhara kwakushindana kwa hoja na kuwaeleza wananchi miradi ya maendeleo ambayo imetekelezwa na Rais Samia Suluhu Hassan.

“Mikutano ya hadhara imefunguliwa vijana ndiyo Askari wa Chama tumlinde Rais wetu kwa hoja na siyo matusi, wenzetu wakitoa matusi, sisi tushindane kwa hoja,”amesema Mlao.

Naye Mwenyekiti wa (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Clement Madinda, amesema maagizo yote yaliyotolewa na MNEC huyo, watayafanyia kazi ikiwamo kuendelea kutumia fursa ya kupata mikopo ya Halmashauri asilimia 10 na kuanzisha miradi ya kiuchumi.

Amesema wanaishukuru pia Serikali kwa kuendelea kuwa amini vijana na hata kuwapatia mikopo, ambapo katika Manispaa ya Shinyanga vijana wamepewa Coaster Mbili, Pikipiki 30, na Trekta mbili kwa upande wa Kahama, huku akiiomba Serikali kuwapatia pia vijana elimu ujasiriamali na usimamizi wa miradi.

Kwa upande wake Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko, amewataka vijana kuendelea kuchangamkia fursa za mikopo asilimia 10 ambayo hutolewa asilimia 4 kwa vijana, na kubainisha Manispaa hiyo katika mwaka wa fedha (2021-2022) imeshatoa kiasi cha fedha Sh.milioni 126 fedha za mikopo kwa vijana.
Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akizungumza kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM mkoani Shinyanga.

Mwenyekiti wa UVCCM Mkoani Shinyanga Clement Madinda akizungumza kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Anorld Makombe akizungumza kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko akizungumza kwenye Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Katibu wa (UVCCM) Mkoa wa Shinyanga Raphael Nyandi akizungumza kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, (katikati) akiwa na Mwenyekiti wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga Clement Madinda na Mjumbe wa Baraza Kuu la CCM Taifa kupitia umoja wa vijana (UVCCM) kutoka mkoa wa Shinyanga Mwanalisa Faustine kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Shinyanga Mjini Anorld Makombe, (kushoto) akiwa na Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.
Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.

Maadhimisho ya miaka 46 ya CCM yakiendelea.
 
 Watoto wenye ulemavu ambao wanalelewa kituo cha Buhangija Manispaa ya Shinyanga wakipokea msaada wa vitu mbalimbali.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, (wapili kutoka kulia) akiendesha baiskeli kuelekea kwa balozi wa tawi la CCM Shina namba 2 Mwajuma Ramadhani na kupandisha Bendera ya Chama.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akipandisha Bendera ya Chama.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akipanda Mti katika Shule mpya ya Sekondari Lubaga.

Mwenyekiti wa UVCCM mkoa wa Shinyanga Clement Madinda akipanda mti katika Shule mpya ya Sekondari Lubaga.

Mjumbe wa Baraza Kuu la CCM Taifa kupitia umoja wa vijana (UVCCM) kutoka Mkoa wa Shinyanga Mwanalisa akipanda mti katika Shule mpya ya Sekondari Lubaga.

Katibu wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga Raphael Nyandi akipanda mti katika shule mpya ya Sekondari Lubaga.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akisalimiana na Mwenyekiti wa CCM wilaya ya Shinyanga Mjini Anorld Makombe alipowasili mkoani Shinyanga kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akisalimiana Meya wa Manispaa ya Shinyanga Elias Masumbuko, alipowasili mkoani Shinyanga kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akisalimiana na Naibu Meya wa Manispaa ya Shinyanga Ester Makune, alipowasili mkoani Shinyanga kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akisalimiana na Katibu wa UVCCM Mkoa wa Shinyanga Raphael Nyandi, alipowasili mkoani Shinyanga kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akisalimiana na Katibu wa Hamasa Mkoa wa Shinyanga Severine Luhende,alipowasili mkoani Shinyanga kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Taifa (NEC) kupitia kundi la vijana (UVCCM) Ramadhani Mlao, akiwa mkoani Shinyanga kwenye maadhimisho ya miaka 46 ya CCM.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments