MWANAFUNZI WA CHUO KIKUU MoCU AJIUA KISA KUKATALIWA NA MREMBO ALIYEMLIPIA KODI NA KUMNUNULIA IPHONE

 Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Ushirika Moshi (MoCU), Gunze Luhangija aliyekuwa akisomea Shahada ya Menejimenti ya Ushirika na Uhasibu (BCMA), amekutwa amejinyonga chanzo kikisemekana ni kutokana na msongo wa mawazo uliosababishwa na kukataliwa na mpenzi wake.


Inadaiwa alishawahi kujaribu kujiua kwa kunywa sumu Januari 4 mwaka huu lakini aliokolewa baada ya kukataliwa ilihali ikieleza kuwa alimgharamikia mpenzi wake huyo ikiwemo kumpangishia nyumba.

Baadhi ya wanafunzi kutoka chuoni hapo wamedai marehemu alikuwa na ugomvi na mpenzi wake siku chache baada ya kumnunulia simu janja aina ya iPhone 14 iliyopelekea kuwa katika hali ya msongo wa mawazo.

“Siku ya Boxing Day alimnunulia mpenzi wake iPhone 14 na baada ya siku chache demu (mpenzi) alimkataa kwamba kapata mtu mwingine [..] dogo kajitundika,” mmoja wa wanafunzi chuoni hapo.

Aidha, Kaimu Kamanda wa Polisi mkoani Kilimanjaro, Yahya Mdogo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa jeshi linaendelea na uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo chake.


Via: Swahili Times


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments