AFISA UHIFADHI WANYAMAPORI SERENGETI AUAWA KWA KUPIGWA MSHALE WENYE SUMU


Afisa uhifadhi wa wanyamapori daraja la kwanza wa hifadhi ya Taifa ya Serengeti, Deus Mwakajegele ameuawa kwa kuchomwa mshale na watu wasiojulikana alipokuwa akitekeleza majukumu yake ya kulinda hifadhi ya Serengeti Mkoani Mara.


Tukio hilo limetokea jana Jumamosi Januari 21, 2023 katika eneo la Nyanungu wilayani Tarime baada ya kuchomwa mshale wenye sumu kichwani na kufariki katika hospitali ya Seliani Arusha alipopelekwa kwa ajili ya matibabu.

Mkuu wa Mkoa wa Mara, Meja Jenerali Suleiman Mzee amesema kuwa tukio hilo limetokea katika eneo lililokuwa na mgogoro ambao ulikuwa umetolewa maamuzi na vyombo vya dola.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments