AJALI YAUA WATU SITA WA FAMILIA MOJA BOXING DAY


Familia ya watu sita akiwemo baba, Khumbulani Togara, mama na watoto wao wanne, akiwemo kichanga, wamefariki dunia katika ajali ya kutisha iliyotokea siku ya Boxing Day, Desemba 26, 2022.

Ajali hiyo iliyozua gumzo kubwa na kuwasikitisha wengi, imetokea nchini Afrika Kusini katika eneo la Musina, wakati familia hiyo ikirejea nyumbani kwao, Zimbabwe baada ya kula Krismasi nchini Afrika Kusini.


Video iliyonaswa na kamera za CCTV, imenasa tukio hilo ambapo familia hiyo ikiwa ndani ya gari aina ya Mitsubishi ‘double cabin’, ilivaana uso kwa uso na lori lililokuwa kwenye spidi kubwa na kusababisha maafa hayo.
Ajali hiyo imetokea katika Barabara ya N1 kati ya Miji ya Baobab Tollgate na Musina.

Inaelezwa kuwa chanzo cha ajali hiyo, ni uchovu na mwendokasi.

Taarifa hiyo iliripotiwa pia na Ubalozi wa Zimbabwe nchini Afrika Kusini kupitia kwa Balozi Melody Chaurura


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments