POLISI ALIYEOA MWEZI ULIOPITA AFUMANIWA AKICHEPUKA NA MKE WA MTU


Polisi

Afisa wa polisi nchini Kenya aliyefunga ndoa Desemba mwaka jana, amefumaniwa chumbani akiwa na mke wa mtu, katika nyumba moja mtaa wa Eastlands jijini Nairobi.

Mwanamume huyo aliyemfumania Afisa wa Polisi, imeelezwa kwamba alikuwa amesafiri kwenda kijijini na aliporudi nyumbani akamkuta mkewe akimsaliti.

Baada ya majibizano ya muda mfupi, mwanaume ambaye amefahamika kwa jina la Ali Abdul Majid, alihisi kutishiwa maisha na kuamua kupiga ripoti katika Kituo cha Polisi cha Dondora.

Maafisa wenzake mtuhumiwa waliotoa michango katika sherehe yake ya harusi walishangazwa kabisa na kisa hicho.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments